1Zaburi ya Daudi.
Ee Yawe,
nani atakayekaa katika hema yako?
Nani atakayeishi juu ya mulima wako mutakatifu?
2-5Ni mutu anayefanya hivi:
anaishi katika ukamilifu,
anatenda kwa haki siku zote,
anasema ukweli kutoka ndani ya moyo,
hatetani,
hatendei rafiki yake uovu,
hamutukani jirani yake,
anazarau wapotevu,
anaheshimu wanaomwabudu Yawe,
hageuzi kiapo chake hata kikimuletea hasara,
hakopeshi feza yake kwa kupata faida,
wala kupokea kituliro kumutesa asiyekuwa na kosa.
Mutu anayefanya vile,
hatatikisika hata kidogo.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.