1Mukusanyike, mukusanyike, enyi taifa la watu wasiokuwa na haya,
2mbele hamujapeperushwa mbali kama maganda,
mbele haijawafikia siku ya hasira kali ya Yawe,
mbele haijawafikia siku ya kasirani ya Yawe.
3Mutafute Yawe, enyi wanyenyekevu wote katika inchi,
enyi munaozitii amri zake.
Mutafute haki, mutafute unyenyekevu;
labda mutaiponyoka siku ya kasirani ya Yawe.
Maangamizi kwa mataifa jirani4Muji wa Gaza utahamwa,
muji wa Askeloni utakuwa tupu.
Wakaaji wa Asidodi watafukuzwa muchana,
na wale wa Ekroni wataongolewa.
5Ole wenu wakaaji wa inchi za pembeni ya bahari,
watu wanaoishi kule Krete!
Yawe amesema juu yenu,
enyi wakaaji wa Kanana, inchi ya Wafilistini:
Mimi nitawaangamiza wala hakutabaki hata mukaaji mumoja!
6Nanyi inchi ya pembeni ya bahari mutafanywa kuwa shamba la malisho;
mutakuwa vibanda vya wachungaji
na mazizi ya kondoo.
7Inchi ya pembeni ya bahari itakuwa makao ya mabaki ya ukoo wa Yuda.
Watachunga nyama wao kule.
Nyumba za muji wa Askeloni
zitakuwa pahali pao pa kulala.
Maana mimi Yawe, Mungu wao nitawakumbuka
na kuwarudishia hali yao njema.
8Nimeyasikia matusi ya Wamoabu
na mazarau ya Waamoni,
jinsi walivyowatusi watu wangu
na kujivuna kwamba wamenyanganya inchi yao.
9Kwa hiyo, kama vile ninavyoishi,
–ni ujumbe wa Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli–
inchi ya Moabu itakuwa kama Sodoma
na ya Amoni itakuwa kama Gomora.
Inchi zake zitakuwa shamba la miiba na mashimo ya chumvi,
zitakuwa ukiwa milele.
Watu wangu watakaobaki wataziteka,
watu wa taifa langu waliobaki watazirizi.
10Hayo yatakuwa malipo ya kiburi chao,
kwa sababu waliwachekelea na kujivuna
mbele ya watu wa Yawe wa majeshi.
11Wao watamwogopa sana Yawe;
ataiangamiza miungu yote ya dunia.
Mataifa yote katika dunia yatamwabudu;
kila taifa katika pahali pake.
12Nanyi watu wa Kushi vilevile
mutauawa kwa upanga.
13Yawe atanyoosha mukono wake
kwa kuazibu inchi ya upande wa kaskazini,
na kuiangamiza inchi ya Asuria.
Ataufanya muji wa Ninawe kuwa ukiwa,
kuwa pahali penye kukauka kama jangwa.
14Makundi ya nyama wa kufugwa watalala ndani yake,
vilevile kila nyama wa pori.
Tai, nyangenyange na korongo wataishi juu ya nguzo zake,
bundi watalia kwenye madirisha yake,
vibombobombo watalia kwenye vizingiti,
maana nyumba zake za mierezi zitakuwa tupu.
15Basi huu ndio muji uliojivuna na kuishi kwa usalama,
muji uliojisemesha: Ni mimi tu, hakuna mwingine!
Jinsi gani umekuwa mutupu
na makao ya nyama wa pori!
Kila mutu anayepita karibu atauzomea na kuuzarau.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.