1Ninyi watoto muwatii wazazi wenu mbele ya Bwana, kwa maana vile ndivyo inavyostahili.
2“Heshimu baba yako na mama yako.” Hii ni amri ya kwanza ambayo waliongeza ahadi hii juu yake:
3“Kusudi upate heri na uishi siku nyingi katika dunia.”
4Na ninyi wababa musiwakasirikishe watoto wenu. Lakini muwalee na kuwaonya, mukiwatolea mashauri yanayotoka kwa Bwana.
Maonyo kwa watumwa na wabwana wao5Ninyi watumwa, mutii wabwana wenu kwa woga na kutetemeka na kwa moyo wa ukweli kama vile munavyomutumikia Kristo.
6Musitumike tu wakati wanapowaangalia, mukitafuta kuwapendeza. Lakini mutimize mapenzi ya Mungu kwa moyo wote mukijihesabu kama watumwa wa Kristo.
7Mufanye kazi yenu ya utumwa kwa moyo mwema, kama vile wenye kumutumikia Bwana, wala si watu tu.
8Mukumbuke kwamba Bwana atalipa kila mutu sawa na matendo yake mema, akiwa huru au mutumwa.
9Na ninyi wabwana muwatendee watumwa wenu hivi vilevile. Muache kuwatisha, mukijua kwamba ninyi na watumwa wenu muko na Bwana mumoja mbinguni, naye hafanyi kitu kwa upendeleo.
Silaha za kiroho10Basi kwa kumaliza, musimame imara katika kuungana kwenu na Bwana kwa uwezo wa nguvu zake kubwa.
11Muvae silaha zote Mungu anazowapa, kusudi mupate kushinda mayele ya Shetani.
12Kwa maana hatupigani na watu wa dunia hii, lakini tunapigana na pepo mbaya zinazokaa katika eneo la mbingu pamoja na wakubwa, na wenye mamlaka na watawala wa dunia hii ya giza.
13Kwa hiyo sasa mutwae silaha zote Mungu anazowapatia. Kwa njia hii mutaweza kushinda adui yenu siku mbaya itakapowafikia. Nanyi mutakapokwisha kumaliza mapigano, mutaweza kusimama imara.
14Basi, mujiweke tayari: mukijifungia ukweli kama vile mukaba, mukivaa haki kama vile nguo ya chuma ya kukingia kifua,
15na mukuwe na bidii ya kutangaza Habari Njema ya amani kama vile viatu munavyovaa.
16Na zaidi ya hivi vyote, muchunge imani kama vile munavyoshika ngao, kusudi mupate kuzimisha mishale yote yenye moto ya yule Mwovu.
17Mupokee wokovu kama vile kofia ya chuma ya kuwalinda, na Neno la Mungu kama upanga munaopewa na Roho.
18Mumwombe Mungu kila wakati mukiongozwa na Roho. Mumwombe na kumusihi kwa kila namna. Kwa hiyo mukeshe bila kuchoka mukiwaombea watu wote wa Mungu.
19Muniombee vilevile, kusudi Mungu anijalie maneno ya kusema. Kwa hiyo nitaweza kuwajulisha watu kwa uhodari siri ya Habari Njema.
20Mimi ni mujumbe wa Habari ile Njema, ijapokuwa sasa ninakuwa katika kifungo. Basi muniombee kusudi nipate kusema kwa uhodari, sawa inavyonipasa kusema.
Salamu za mwisho21Tikiko, ndugu yetu mupendwa na mutumishi mwaminifu wa Bwana atawapasha habari zangu zote, kusudi mupate kujua kama mimi ni katika hali gani na namna kazi inavyoendelea.
22Ni kwa shabaha hiyo ninamutuma kwenu, apate kuwajulisha habari zetu na kuwafariji.
23Ninawatakia wandugu amani, upendo na imani kutoka kwa Mungu Baba na kwa Bwana Yesu Kristo.
24Ninawatakia neema wale wote wanaomupenda Bwana wetu Yesu Kristo kwa upendo usiokuwa na mwisho.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.