1Hawa ndio wafalme ambao Waisraeli waliwashinda na kunyanganya inchi yao yote iliyokuwa upande wa mashariki wa muto Yordani kutokea bonde la muto Arnoni mpaka kwenye mulima Hermoni na inchi yote ya Araba upande wa mashariki:
2Mufalme Sihoni wa Waamori aliyeishi kule Hesiboni na kutawala kutokea kwenye makao yake makubwa kule Aroeri, muji uliokuwa kandokando ya bonde la Arnoni. Alitawala vilevile kuanzia katikati ya bonde mpaka kwenye muto Yaboki ambao ulikuwa mupaka wa inchi ya Waamoni, ni kusema nusu ya inchi ya Gileadi.
3Vilevile, alitawala inchi yote ya Araba, kutokea bahari ya Kineroti, upande wa mashariki, mpaka Beti-Yesimoti kwenye bahari ya Chumvi na kuendelea mpaka chini ya mulima Pisiga.
4Mwingine ni mufalme Ogi mumoja wa Warefaimu waliobaki, ambaye alitawala Basani na alikaa Asitaroti au Edirei.
5Utawala wake ulienea mpaka kule kwenye mulima Hermoni, kule Saleka, Basani yote mpaka kwa mipaka ya Wagesuri na Wamakati, nusu ya Gileadi hata kwa mupaka wa inchi ya mufalme Sihoni wa Hesiboni.
6Musa mutumishi wa Yawe pamoja na Waisraeli aliwashinda wafalme hao, akawapatia inchi hizo makabila ya Rubeni, Gadi na nusu ya kabila la Manase zikuwe mali yao kabisa.
7Kisha Yoshua pamoja na Waisraeli waliwashinda wafalme wote wa eneo lote linalokuwa upande wa magaribi wa muto Yordani, kuanzia Bali-Gadi katika bonde la Lebanoni mpaka kwenye mulima uliokuwa mutupu wa Halaki upande wa kusini karibu na Seiri. Yoshua akayagawanyia makabila ya Israeli inchi hizo zikuwe mali yao kabisa.
8Inchi hizo zilikuwa pamoja na maeneo ya milima, inchi ya bonde, eneo la Araba, miteremuko ya milima, maeneo ya jangwa, na eneo la Negebu; inchi zilizokuwa za Wahiti, Waamori, Wakanana, Waperizi, Wahivi na Wayebusi.
9Wafalme walioshindwa walikuwa, mumoja kwa mwengine:
mufalme wa Yeriko, mufalme wa Ai muji unaokuwa karibu na Beteli,
10mufalme wa Yerusalema, mufalme wa Hebroni,
11mufalme wa Yarmuti, mufalme wa Lakisi,
12mufalme wa Eguloni, mufalme wa Gezeri,
13mufalme wa Debiri, mufalme wa Gederi,
14mufalme wa Horma, mufalme wa Aradi,
15mufalme wa Libuna, mufalme wa Adulamu,
16mufalme wa Makeda, mufalme wa Beteli,
17mufalme wa Tapua, mufalme wa Heferi,
18mufalme wa Afeki, mufalme wa Lasaroni,
19mufalme wa Madoni, mufalme wa Hazori,
20mufalme wa Simuroni-Meroni, mufalme wa Akisafu,
21mufalme wa Tanaki, mufalme wa Megido,
22mufalme wa Kedesi, mufalme wa Yokinamu muji unaokuwa kwenye mulima Karmeli,
23mufalme wa Dori katika sehemu ya Nafoti-Dori, mufalme wa Goyimu kule Gilgali na
24mufalme wa Tirza.
Jumla ya wafalme hao ni makumi tatu na mumoja.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.