1Basi sasa tuseme nini? Tuendelee kuishi katika zambi kusudi neema ya Mungu izidi kuongezeka?
2Hapana hata kidogo! Sisi tuliokufa kwa ajili ya zambi, namna gani tutaweza tena kuishi katika zambi?
3Munajua hakika kwamba sisi wote tulipobatizwa tuliungana na Yesu Kristo; kwa njia hiyo tuliungana naye katika kufa.
4Hivi, kwa njia ya ubatizo, tuliungana naye katika kufa na katika kuzikwa kwake, kusudi kama vile Kristo alivyofufuliwa kwa uwezo wenye utukufu wa Baba, sisi vilevile tupate kuishi katika maisha mapya.
5Ikiwa tuliungana naye kwa njia ya kufa kama yeye, tutaungana naye vilevile kwa njia ya kufufuliwa kama yeye.
6Kwa maana tunajua kwamba ule utu wetu wa zamani ulitundikwa pamoja na Kristo, kusudi tusitawaliwe tena na hiyo tabia ya zambi na tusikuwe tena watumwa wa zambi.
7Kwa sababu mutu akikufa anapata uhuru toka katika zambi.
8Ikiwa tumekufa pamoja na Kristo, tunaamini kwamba tutaishi pamoja naye vilevile.
9Kwa maana tunajua kwamba Kristo amefufuliwa, naye hawezi kufa tena, kwa sababu kifo hakina tena uwezo juu yake.
10Kuelekea jambo la kufa kwake, alikufa mara moja tu kwa ajili ya zambi; lakini kuelekea maisha yake, sasa anaishi kwa ajili ya Mungu.
11Hivi vilevile mujihesabu kuwa mumekufa kwa ajili ya zambi na kuwa munaishi pamoja na Mungu mukiungana na Yesu Kristo.
12Basi musiache tena zambi kutawala katika mwili wenu wa kufa, hata mupate kufuata tamaa zake mbaya.
13Musitoe tena viungo vya mwili wenu kufanya zambi, mukivitumikisha kama vyombo vya kufanya mabaya. Lakini mujitoe wenyewe kwa kumutumikia Mungu kama watu waliofufuliwa na mutumikishe viungo vya mwili wenu kama vyombo vya kufanya haki.
14Kwa maana hamutatawaliwa tena na zambi, kwa sababu hamuishi chini ya uongozi wa Sheria lakini chini ya uongozi wa neema ya Mungu.
Watumwa wa uhaki15Ni nini basi? Tufanye zambi kwa sababu sisi hatuishi chini ya Sheria, lakini chini ya uwongozi wa neema ya Mungu? Hapana hata kidogo!
16Munajua hakika kwamba mukijitoa wenyewe kwa mutu fulani kuwa watumwa wake na kulazimishwa kumutii, munakuwa kweli watumwa wa yule munayemutii. Ikiwa ni utumwa wa zambi, mwisho wake ni kifo; ikiwa ni kumutii Mungu, mwisho wake ni maisha ya haki.
17Lakini asante kwa Mungu, kwa maana ninyi muliokuwa zamani watumwa wa zambi mumetii sasa kwa moyo wenu wote kanuni za mafundisho muliyopewa.
18Mumewekwa kuwa huru toka katika utumwa wa zambi, na sasa mumegeuka watumwa wa haki.
19(Ninatumia luga ya kawaida ya wanadamu kwa sababu ya uzaifu wenu wa kimutu). Zamani mulijitoa kabisa kuwa watumwa wa kufanya mambo machafu na maovu kwa kuishi katika machafuko. Hivi vilevile mujitoe kabisa kuwa watumwa wa kufanya haki kusudi muweze kuishi katika utakatifu.
20Wakati mulipokuwa watumwa wa zambi, mulikuwa huru kufuatana na mambo ya haki.
21Basi mulipata faida gani kwa kufanya mambo yale munayopata haya juu yake sasa? Maana mwisho yao ni kifo!
22Lakini sasa kufuatana na vile mumewekwa huru toka utawala wa zambi na kugeuka watumwa wa Mungu, munapata faida ya kuishi katika utakatifu na kwa mwisho kupewa uzima wa milele.
23Kwa maana mushahara wa zambi ni kifo, lakini zawadi Mungu anayotoa ni uzima wa milele kwa kuungana na Yesu Kristo, Bwana wetu.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.