1Ita sasa, uone kama kuna wa kukuitikia.
Ni nani kati ya watakatifu utakayemwita?
2Kweli mahangaiko yanamwua mupumbafu,
na wivu unamwangamiza mujinga.
3Nimepata kuona mupumbafu akistawi,
lakini kwa rafla nikalaani makao yake.
4Watoto wake hawana usalama.
Wanaonelewa katika tribinali,
na hakuna mutu wa kuwatetea.
5Mazao yake yanakuliwa na wenye njaa,
hata ngano iliyoota kati ya miiba.
Wenye tamaa wananyanganya utajiri wake.
6Kwa kawaida mateso hayatoki katika mavumbi,
wala matatizo hayachipuki katika udongo.
7Lakini mwanadamu anazaliwa apate taabu,
kama vile cheche za moto zinavyoruka juu.
8Kwa ngambo yangu, mimi ningemugeukia Mungu,
ningemutolea Mungu maneno yangu,
9yeye anayetenda mambo makubwa yasiyochunguzika,
anayetenda maajabu yasiyohesabika.
10Ananyeshea inchi mvua,
anapeleka maji katika mashamba.
11Anainua juu wanaokuwa zaifu;
wenye kuomboleza anawapa usalama.
12Anavunja mipango ya wadanganyifu,
matendo yao yasipate mafanikio.
13Anawanasa wenye hekima kwa werevu wao,
anakomesha mara moja mipango ya waovu.
14Wao wanapatwa na giza wakati wa muchana;
muchana kati wanapapasapapasa kama vile usiku.
15Lakini Mungu anawaokoa wayatima wasiuawe,
anawaponyesha wakosefu toka katika mikono ya wenye nguvu.
16Hivyo wamasikini wanapata tumaini,
nao uovu unakomeshwa.
17Heri mutu yule anayeazibiwa na Mungu!
Hivyo usizarau Mungu Mwenye Uwezo anapokuazibu.
18Maana yeye anaumiza na tena anatunza,
anatia kidonda na kwa mukono wake anaponyesha.
19Atakuokoa mara sita toka katika magumu;
hata mara saba hasara haitakugusa.
20Atakuepusha toka kifo wakati wa njaa,
toka mapigo ya upanga wakati wa vita.
21Utakingwa salama na mashambulio ya ulimi,
wala hautaogopa maangamizi yanapokuja.
22Maangamizi na njaa vinapokuja, utacheka,
wala hautaogopa nyama wakali wa inchi.
23Nawe utapatana na mawe ya shamba,
na nyama wakali watakuwa na amani nawe.
24Utakaa na amani katika nyumba yako;
utachunguza makundi yako ya nyama,
utaona yote iko.
25Utaona vilevile wazao wako watakuwa wengi,
wengi kama majani katika mashamba.
26Utashuka katika kaburi ukiwa na miaka yenye kutimia,
kama vile muganda wa ngano uliokomaa vizuri.
27Basi haya ndiyo mambo tuliyochunguza.
Ni hivi tu.
Uyasikie na kuyaelewa kwa faida yako.
Jibu la YobuWho We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.