1Kwa mukubwa wa waimbaji: kwa mutindo wa watu wa Gati. Zaburi ya Asafu.
2Mumwimbie Mungu kwa sauti, maana ni nguvu yetu,
mumushangilie Mungu wa Yakobo,
3muvumishe wimbo wa shangwe, mupige ngoma,
mucheze zeze na kinubi cha sauti nzuri.
4Mupige baragumu kutangaza mwandamo wa mwezi,
na pia mbalamwezi wakati wa sikukuu yetu.
5Hilo ndilo sharti katika Israeli;
hilo ndilo agizo la Mungu wa Yakobo.
6Aliwapa watu wa Israeli agizo hilo,
aliposhambulia inchi ya Misri.
Ninasikia sauti nisiyoitambua ikisema:
7“Mimi nilikutua mizigo yako toka kwenye mabega,
nilikuondolea matofali uliyochukua katika mikono.
8Katika shida uliniita, nami nikakuokoa.
Nilikujibu kutokea katika ngurumo.
Nilikujaribu kwenye maji ya Meriba.
9Enyi watu wangu, musikie onyo langu.
Heri ungenisikiliza, ee Israeli!
10Usikuwe na mungu wa kigeni;
usiabudu hata kidogo mungu mwingine.
11Mimi ni Yawe, Mungu wako,
niliyekutoa katika inchi ya Misri.
Fungua kinywa chako, nami nitakulisha.
12“Lakini watu wangu hawakunisikiliza;
Israeli hakunitaka kabisa.
13Hivyo, nikawaacha wabaki katika ugumu;
wafuate mashauri yao wenyewe.
14Heri watu wangu wangenisikiliza!
Heri Israeli angefuata njia zangu!
15Ningewashinda waadui zao haraka;
ningenyoosha mukono juu ya wapinzani wao.
16Wanaonichukia wangenipigia magoti kwa hofu,
na azabu yao ingekuwa ya milele.
17Lakini wewe ningekulisha kwa ngano bora,
ningekushibisha kwa asali ya pori.”
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.