1Neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:
2Wewe mwanadamu! Toa unabii juu ya wachungaji wa inchi ya Israeli. Uwaambie hao wachungaji kwamba:
Bwana wetu Yawe anasema hivi: Ole kwenu ninyi wachungaji wa inchi ya Israeli, munaojikulisha ninyi wenyewe tu! Haiwapasi wachungaji kuwakulisha kondoo?
3Munakunywa maziwa, munavaa nguo za manyoya yao na munawachinja kondoo wanono na kuwakula. Lakini hamuwakulishi hao kondoo.
4Wanaokuwa zaifu hamukuwatia nguvu, wagonjwa hamukuwatunza, waliovunjika hamukuwafunga kwa kitambaa, waliotangatanga hamukuwarudisha na waliopotea hamukuwatafuta. Lakini mukawatawala kwa kinguvu na kuwatesa.
5Basi, kwa sababu hao kondoo hawakuwa na muchungaji, walisambazwa na kuwa chakula cha nyama wa pori.
6Kweli, kondoo walisambazwa, wakatangatanga juu ya milima na vilima. Kondoo walisambazwa katika dunia yote, na hakukukuwa mutu aliyejali juu yao wala kuwatafuta.
7Basi, musikie vizuri neno la Yawe, enyi wachungaji:
8Kama vile ninavyoishi, –ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe– nimechoka kuwaona kondoo wangu wamekuwa chakula cha nyama wakali kwa vile hakukukuwa muchungaji; wachungaji wangu hawakuwatafuta kondoo wangu, lakini wamejikulisha wao wenyewe pahali pa kuwakulisha kondoo wangu.
9Basi, ninyi wachungaji, musikie neno la Yawe.
10Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitapingana nanyi, enyi wachungaji. Nitawaondoa madaraka ya kuchunga kondoo wangu, wala sitakubali muwachunge tena. Hamutakuwa tena na nafasi ya kufaidika ninyi wenyewe. Nitawaokoa kondoo wangu toka katika makucha yenu, kusudi wasikuwe chakula chenu tena.
Muchungaji Mwema11Basi, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Mimi mwenyewe nitawatafuta kondoo wangu na kuwatunza.
12Kama muchungaji anavyowatafuta kondoo wake waliosambazwa, ndivyo nitakavyowatafuta kondoo wangu. Nitawarudisha kutoka kila pahali waliposambazwa kwa siku yenye mawingu ya hatari na giza nene.
13Nitawatoa kutoka kwa watu wa mataifa. Nitawakusanya kutoka inchi za mbali na kuwaleta katika inchi yao wenyewe. Nitawachunga juu ya milima ya inchi ya Israeli, kandokando ya vijito na katika sehemu zote za inchi zinazokaliwa na watu.
14Nitawapa malisho mazuri kwenye milima mirefu ya inchi ya Israeli ambako kuna mashamba mazuri ya kuwakulishia. Watapumzika huko kwenye mbuga za malisho mazuri; watapata malisho mazuri juu ya milima ya inchi ya Israeli.
15Mimi mwenyewe nitakuwa muchungaji wa kondoo wangu. Mimi mwenyewe nitawapumzisha.
–Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–
16Nitawatafuta kondoo waliopotea na waliotangatanga nitawarudisha kwa nyumba. Waliovunjika nitawatunza, na wale wanaokuwa zaifu nitawapatia nguvu. Lakini kondoo wanono na wenye nguvu nitawaangamiza. Mimi nitawachunga kondoo kama inavyostahili.
17Bwana wetu Yawe anasema hivi: Kwa ninyi munaokuwa kundi langu, nitaamua kati ya kondoo na kondoo; kati ya kondoo dume na mbuzi.
18Wamoja kati yenu wanakula malisho mazuri na vilevile kukanyagakanyaga yale yaliyobaki. Wanakunywa maji safi na yanayobaki wanayachafua kwa miguu yao!
19Basi, kondoo wangu wengine wakule malisho yaliyokanyagwakanyagwa na kunywa maji yaliyochafuliwa?
20Kwa hiyo, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Mimi mwenyewe nitaamua kati ya kondoo wanono na kondoo zaifu.
21Ninyi munawasukuma kwa mbavu na kwa mabega na kuwapiga pembe kondoo wote wanaokuwa zaifu hata mumewatawanya mbali na kundi.
22Lakini mimi nitawaokoa kondoo wangu wasiendelee tena kuteswa. Nitatoa hukumu juu ya kila kondoo.
23Nitaweka muchungaji mumoja juu yao, mufalme kama mutumishi wangu Daudi. Yeye atawakulisha na kuwa muchungaji wao.
24Nami Yawe, nitakuwa Mungu wao, naye mutumishi wangu Daudi atakuwa mukubwa wao. Ni mimi Yawe ninayesema hivyo.
25Nitafanya nao agano la amani. Nitaondoa nyama wakali katika inchi, kusudi kondoo wangu wakae katika mbuga kwa usalama na kulala katika pori.
26Nitawafanya waishi kandokando ya mulima wangu mutakatifu na kuwabariki. Nitawaletea mvua kwa wakati wake, nazo zitakuwa mvua za baraka.
27Miti inayokuwa katika mashamba itazaa matunda, udongo utatoa mazao kwa wingi, nao wataishi kwa salama katika inchi yao. Nitakapovunja nira zao za utumwa na kuwaokoa toka katika mikono ya hao waliowafanya kuwa watumwa halafu watatambua kwamba mimi ni Yawe.
28Hawatakamatwa tena mateka na mataifa mengine wala nyama wa pori hawatawaua na kuwakula. Wataishi kwa usalama na hakuna atakayewatisha.
29Nitawapa mashamba yenye mboleo kusudi wasiangamizwe tena na njaa katika inchi ile, wala kuzarauliwa tena na mataifa mengine.
30Nao watajua kwamba mimi Yawe, Mungu wao, niko pamoja nao na kwamba watu hao wa inchi ya Israeli ni watu wangu.
31Nanyi, ee kondoo wangu, ninyi ni watu wangu, nami ni Mungu wenu.
–Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.