1Wakati Rehoboamu alipoimarisha utawala wake, yeye pamoja na watu wake wote waliacha kutii Sheria ya Yawe.
2Katika mwaka wa tano wa utawala wake, kwa sababu hawakumutii Yawe, Sisaki, mufalme wa Misri akashambulia muji wa Yerusalema,
3akiwa na magari elfu moja na mia mbili, waaskari wapanda-farasi elfu makumi sita. Alikuwa vilevile na waaskari wengi sana wasioweza kuhesabiwa toka Misri; Walibia, Wasuki na Waetiopia.
4Aliteka miji yenye kuzungukwa na kuta katika Yuda, akafika mpaka Yerusalema.
5Kisha Nabii Semaya akamwendea mufalme Rehoboamu na wakubwa wa Yuda, waliokusanyika Yerusalema ambapo walikimbilia kwa kumwepuka Sisaki, akamwambia: “Yawe anasema hivi: ‘Ninyi mumeniacha mimi, kwa hiyo basi, nami nimewaacha ninyi na kuwatia katika mikono ya Sisaki.’ ”
6Halafu wakubwa wa Israeli na mufalme wakajinyenyekeza, wakasema: “Yawe ni mwenye haki.”
7Yawe alipoona kwamba wamejinyenyekeza, akazungumuza tena na nabii Semaya, akamwambia: “Wamejinyenyekeza, sitawaangamiza, lakini nitawaokoa nyuma ya muda mufupi. Sitashushia muji Yerusalema kasirani yangu na kuuharibu kwa mukono wa Sisaki,
8lakini watamutumikia kusudi wapate kujua tofauti inayokuwa kati ya kunitumikia mimi na kuwatumikia wafalme wa dunia.”
9Basi, mufalme Sisaki wa Misri akashambulia muji Yerusalema, akaichukua hazina yote ya nyumba ya Yawe na ya nyumba ya kifalme, pamoja na ngao za zahabu ambazo mufalme Solomono alizozitengeneza. Ang. 1 Fal 10.16-17; 2 Sik 9.15-16
10Kwa pahali pa ngao hizo, mufalme Rehoboamu akatengeneza ngao za shaba na kuziweka chini ya ulinzi wa walinzi wa mulango wa nyumba ya kifalme.
11Kila wakati mufalme alipokwenda katika nyumba ya Yawe, walinzi waliingia walibeba ngao zile na kisha walizirudisha katika chumba cha ulinzi.
12Alipojinyenyekeza, Yawe akaacha kumukasirikia na hakumwangamiza kabisa. Zaidi ya hayo, hali ya inchi ya Yuda ilikuwa nzuri.
Mwisho wa utawala wa Rehoboamu13Basi mufalme Rehoboamu akajiimarisha zaidi katika Yerusalema, na kutawala Yuda. Alikuwa na umri wa miaka makumi ine na mumoja alipoanza kutawala. Naye alitawala kwa muda wa miaka kumi na saba katika Yerusalema, muji ambao Yawe aliuchagua kati ya makabila yote ya Israeli kusudi aabudiwe ndani yake. Mama ya Rehoboamu aliitwa Nama, kutoka Amoni. Ang. 1 Fal 14.21
14Rehoboamu alitenda maovu, kwa maana hakutayarisha moyo wake kwa kumutafuta Yawe.
15Matendo ya mufalme Rehoboamu tangu mwanzo mpaka ya mwisho yameandikwa katika kitabu cha “Mambo ya Siku ya nabii Semaya”, na “Mambo ya Siku ya nabii Ido.” Wakati huu wote, kulikuwa vita ya mufululizo kati ya Rehoboamu na Yeroboamu.
16Kisha Rehoboamu alikufa na kuzikwa katika muji wa Daudi, na Abiya mwana wake akatawala kwa pahali pake.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.