1Kisha yule mutu alinipeleka kwenye kiwanja cha inje mpaka kwenye jengo lililokuwa upande wa kaskazini, naye akaniingiza kwenye vyumba vinavyoelekea kiwanja cha hekalu na jengo lililokuwa upande wa kaskazini.
2Jengo hili lililokuwa upande wa kaskazini lilikuwa na urefu wa metre makumi tano na upana wa metre makumi mbili na tano.
3Kulikuwa gorofi tatu zilizounganisha metre kumi za kiwanja cha ndani na zikielekea sakafu ya kiwanja cha inje.
4Upande wa kaskazini wa jengo hilo, kulikuwa njia ya kupitia yenye upana wa metre tano na urefu wake metre makumi tano. Milango yake ilikuwa upande wa kaskazini.
5Vyumba katika hatua ya juu vilikuwa vyembamba kuliko vile vya katikati na vya chini maana vilikuwa mbali zaidi.
6Vile vyumba vya juu kabisa vilijengwa kwenye miinuko na havikusaidiwa na nguzo kama majengo mengine kwenye kiwanja cha inje.
7Kulikuwa ukuta mbele ya vyumba kuelekea kiwanja cha inje ukiwa na urefu wa metre makumi mbili na tano.
8Wakati vile vyumba kwenye kiwanja cha inje vikiwa na urefu wa metre makumi mbili, vile vinavyoelekea hekalu vilikuwa na urefu wa metre makumi tano.
9Chini ya vyumba hivi kulikuwa njia ya kupitia tokea upande wa mashariki kwa mwisho wa jengo, ikiwa mutu anaingia tokea kiwanja cha inje
10ambako ukuta wa inje unaanzia.
Kwenye upande wa kusini kulikuwa jengo lingine sawa na lile lingine, si mbali na jengo la upande wa magaribi kwa mwisho wa hekalu.
11Mbele ya vyumba hivyo kulikuwa njia ya kupitia kama ile ya upande wa kaskazini. Jengo hilo lilikuwa na vipimo vilevile kama vya lile lingine, maingilio, magawanyo na milango ilifanana na ile ingine.
12Kulikuwa mulango chini ya vyumba kwenye upande wa kusini wa jengo, kwa mwisho wa upande wa mashariki ambako ukuta ulianzia.
13Yule mutu akaniambia: Vyumba hivi vyote ni vitakatifu. Ndani ya vyumba hivi makuhani wanaoingia mbele ya Yawe, wanakula sadaka takatifu kabisa: sadaka takatifu kabisa na humo ndimo munamowekwa sadaka za vyakula, sadaka za kuomba kusamehewa zambi na sadaka kwa ajili ya malipo ya kosa kwa sababu pahali hapo ni patakatifu.
14Makuhani ambao watakuwa wakitumika katika Pahali Patakatifu, wanapotaka kwenda kwenye kiwanja cha inje, ni lazima waache humo nguo zao walizovaa walipokuwa wanatumika mbele ya Yawe kwa sababu nguo hizo ni takatifu. Ni lazima wavae nguo zingine mbele ya kutoka inje ambako watu wanakusanyika.
Vipimo vya eneo la hekalu15Mutu yule alipokwisha kupima eneo la ndani la nyumba ya Yawe, alinitoa inje kupitia mulango wa mashariki na kulipima eneo la inje.
16Alitwaa ule ufito wake wa kupima na kuupima upande wa mashariki, nao ulikuwa metre mia mbili makumi tano.
17Akaupima upande wa kaskazini kwa kutumia ufito wake, nao ulikuwa metre mia mbili makumi tano.
18Kisha akaupima upande wa kusini kwa kutumia ufito wake, nao ulikuwa metre mia mbili makumi tano.
19Kisha akageuka na kupima upande wa magaribi kwa kutumia ufito wake, nao ulikuwa metre mia mbili makumi tano.
20Hivyo akakuwa amepima pande zote, nazo zilikuwa metre mia mbili makumi tano kila upande. Ukuta huo ulitenganisha kati ya eneo takatifu na lile la kawaida.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.