1Kisha Yesu na wanafunzi wake wakafika kule ngambo ingine ya ziwa la Galilaya katika inchi ya Wagerasi.
2Yesu alipotoka ndani ya chombo, pale pale mutu mumoja aliyeshikwa na pepo akakuja kukutana naye akitoka kwenye makaburi.
3Makao ya mutu huyu yalikuwa katika makaburi, wala hakuna mutu aliyeweza kumufunga tena hata na minyororo.
4Mara nyingi miguu yake ilifungwa vifungo vya chuma, nayo mikono yake na minyororo, lakini alikata minyororo ile na kuvunjavunja vile vifungo vya chuma. Hakuna mutu aliyekuwa na nguvu ya kumushinda.
5Saa zote, usiku na muchana alitangatanga katikati ya makaburi na kwenye milima, akilalamika na kujiumizaumiza kwa mawe.
6Alipomwona Yesu kwa mbali, akaenda mbio na kumupigia magoti
7na kulalamika kwa nguvu, akisema: “Yesu, Mwana wa Mungu Mukubwa, kuna neno kati yako na mimi? Ninakusihi kwa jina la Mungu, usinitese!”
8(Alisema hivi kwa sababu Yesu alikuwa akimwamuru: “Wewe pepo, toka ndani ya mutu huyu!”)
9Basi Yesu akamwuliza: “Jina lako nani?”
Naye akamujibu: “Jina langu ni ‘Jeshi’, maana sisi ni wengi.”
10Akazidi kumusihi Yesu kwamba asiwatoshe wale pepo katika inchi ile.
11Na pale karibu na mulima kulikuwa kundi kubwa la nguruwe wakijitafutia chakula.
12Basi pepo wakamusihi Yesu kwamba awatume kuingia ndani ya nguruwe wale.
13Yesu akawaruhusu. Halafu wale pepo wakatoka ndani ya mutu yule na kuingia ndani ya nguruwe. Kundi zima la nguruwe, karibu elfu mbili, wakatelemuka mbio kwenye mulima na kutumbukia ndani ya ziwa, nao wakazama ndani ya maji.
14Wachungaji wa nguruwe wakaenda mbio kupasha habari katika muji na katika vijiji. Watu wakakuja kusudi waone jambo lililotokea.
15Walipomufikia Yesu, wakamwona yule aliyekuwa na kundi la pepo ndani yake akiikaa, akiwa amevaa nguo nayo akili yake ikiwa sawa. Basi watu wale wakaogopa.
16Nao walioona yale yaliyotendeka wakawaelezea watu wale mambo yaliyomutokea yule aliyekuwa na pepo na yaliyotokea nguruwe.
17Kwa hiyo wakaanza kumusihi Yesu aondoke katika inchi yao.
18Yesu alipokuwa akiingia katika chombo, yule aliyekuwa na pepo akamusihi aende pamoja naye.
19Yesu hakumuruhusu, lakini akamwambia: “Kwenda kwako kwenye jamaa yako, na uwaelezee mambo Bwana aliyokutendea na namna alivyokuhurumia.”
20Basi yule mutu akajiendea, akaanza kutangaza mambo yote Yesu aliyomutendea katika inchi ya Miji Kumi. Na watu wote waliomusikia wakashangaa sana.
Binti ya Yairo na mwanamuke aliyegusa nguo ya Yesu(Mat 9.18-26; Lk 8.40-56)21Yesu akavuka ngambo ingine ya ziwa la Galilaya. Alipokuwa pembeni ya ziwa, watu wengi wakakusanyika karibu naye.
22Halafu mukubwa mumoja wa nyumba ya kuabudia aliyeitwa Yairo, akafika pale. Alipomwona Yesu, akajitupa mbele yake,
23akamusihi sana, akisema: “Binti yangu mudogo yuko karibu kufa. Ninakuomba ukuje kwanza kwa kuweka mikono yako juu yake, kusudi apate kupona na kuishi!”
24Basi Yesu akaenda pamoja naye. Watu wengi walimufuata na kumusongasonga.
25Na kati yao kulikuwa mwanamuke mumoja mwenye ugonjwa wa kutokwa na damu kwa muda wa miaka kumi na miwili.
26Aliwaendea waganga wengi, lakini ingawa vile aliteswa sana na kupoteza mali yake. Yeye hakuweza kupona, lakini hali yake iliendelea kuwa mbaya zaidi.
27Wakati mwanamuke yule aliposikia habari za Yesu, alikuja na kuingia katikati ya kundi la watu nyuma ya Yesu na kugusa nguo yake,
28kwa sababu alikuwa akijisemesha: “Kama nikiweza tu kugusa nguo ya Yesu nitapona.”
29Alipogusa nguo ya Yesu, mara moja damu yake ikaacha kutoka, naye akajisikia amepona.
30Na mara moja Yesu akatambua kama nguvu zilitoka ndani yake. Basi akageuka kati ya kundi na kuuliza: “Ni nani aliyegusa nguo yangu?”
31Wanafunzi wake wakamujibu: “Hauoni namna watu wanavyokusongasonga? Namna gani unauliza kwamba ni nani aliyekugusa?”
32Lakini Yesu akaangalia pande zake zote kusudi amwone yule aliyefanya vile.
33Yule mwanamuke akaogopa na kuanza kutetemeka, kwa sababu alitambua yote yaliyomutukia. Halafu akakuja kujitupa kwa miguu yake na kumwambia ukweli wote.
34Yesu akamwambia: “Binti yangu, imani yako imekuponyesha. Ujiendee na amani, ugonjwa wako umepona!”
35Yesu alipokuwa hajamaliza kusema maneno haya, wajumbe wakafika kutoka kwa yule mukubwa wa nyumba ya kuabudia na kumwambia: “Binti yako amekwisha kufa. Basi kwa sababu gani ungali unamusumbua Mwalimu?”
36Lakini Yesu hakuangalia maneno yao, akamwambia yule mukubwa: “Usiogope, uamini tu.”
37Na Yesu hakuruhusu mutu kumusindikiza, isipokuwa Petro, Yakobo, na Yoane, yule ndugu wa tumbo wa Yakobo.
38Walipofika kwa nyumba ya mukubwa Yairo, Yesu akakuta kuko makelele, nao watu wakilia na kulalamika sana.
39Akaingia ndani ya nyumba, akawaambia: “Kwa nini munafanya makelele na kulia? Mutoto hakukufa, lakini analala tu!”
40Nao wakaanza kumuchekelea. Halafu Yesu akawaondosha wote inje, akawakamata wazazi wa yule mutoto na wanafunzi wake watatu, akaingia katika chumba pahali mutoto alipokuwa.
41Akashika mukono wa mutoto, akamwambia: “Talita kumu,” maana yake: “Kijana binti, ninakuambia, amuka!”
42Mara moja yule kijana akasimama na kuanza kutembea (alikuwa na umri wa miaka kumi na miwili). Nao watu wakashangaa sana kwa kuona jambo hilo.
43Lakini Yesu aliwaagiza sana wasimwambie mutu yeyote jambo lililofanyika. Kisha akawaambia wamupe mutoto yule chakula.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.