Nehemia 9 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Watu wanaungama zambi zao

1Siku ya makumi mbili na ine ya mwezi ule wa saba, watu wa Israeli wakakusanyika, wakifunga kula na kuvaa nguo za magunia na kujipakaa udongo juu ya kichwa kwa kuonyesha majuto juu ya zambi zao.

2Wakati ule, walikuwa wamejitenga mbali na watu wa mataifa mengine, wakasimama na kuungama zambi zao na maovu ya babu zao.

3Kwa muda wa yapata saa tatu, walisimama wakati Sheria ya Yawe, Mungu wao, ikisomwa. Na kwa saa tatu zilizofuata, walikuwa wakitubu na kumwabudu Yawe, Mungu wao.

4Kuliwekwa daraja la Walawi; pale kulisimama Yesua, Bani, Kadimieli, Sebania, Buni, Serebia, Bani na Kenani. Wakamwomba kwa sauti kubwa Yawe, Mungu wao.

5Walawi, ni kusema Yesua, Kadimieli, Bani, Hasabuea, Serebia, Hodia, Sebania na Petahia, wakawaambia watu: Musimame na kumusifu Yawe, Mungu wenu.

Mumusifu milele na milele!

Na watu wakasifu jina lako tukufu,

ambalo linatukuka kuliko baraka na sifa zote.

Maombi ya usamehe wa zambi

6Ezra akaomba akisema:

Wewe peke yako ndiwe Yawe!

Ulifanya mbingu na jeshi lake lote,

dunia na vyote vinavyokuwa ndani yake,

bahari na vyote vinavyokuwa ndani yake.

Unavipatia uzima,

na jeshi lote la mbinguni linakuabudu wewe.

7Wewe ndiwe Yawe,

Mungu uliyemuchagua Abramu.

Ukamutoa toka Uri ya Wakaldea

na kumupa jina la Abrahamu.

8Ukamwona kuwa wa haki mbele yako;

ukafanya agano naye kuwapa wazao wake inchi ya Wakanana,

Wahiti, Waamori, Waperizi, Wayebusi na Wagirgasi.

Na ahadi yako ukaitimiza;

maana wewe ni mwaminifu.

9Uliyaona mateso ya babu zetu

walipokuwa katika inchi ya Misri,

na walipokuomba musaada kwenye bahari Nyekundu

ukawasikiliza.

10Ulifanya miujiza na maajabu mbele ya Mufalme wa Misri,

watumishi wake wote

na watu wote wa inchi yake;

maana ulijua kwamba

waliwagandamiza babu zetu.

Ukajipatia utukufu unaokuwa mpaka leo.

11Uligawanya bahari katikati mbele yao,

nao wakapita katikati ya bahari,

pahali pakavu.

Lakini ukawatupa Wamisri

waliowafuatilia kama jiwe zito

ndani ya maji mengi.

12Muchana uliwaongoza kwa nguzo la wingu,

na usiku uliwaongoza kwa nguzo la moto

kwa kuwaangazia njia ya kufuata.

13Kule kwa mulima Sinai

ulishuka toka mbinguni na kuzungumuza nao.

Ukawapa maagizo safi, sheria za kweli,

masharti mazuri na amri.

14Kwa njia ya Musa, mutumishi wako,

ukawajulisha siku zako za Sabato takatifu

na ukawaagiza kuzifuata amri,

masharti na sheria ulizowaamuru.

15Walipokuwa na njaa,

ukawapa chakula kutoka mbinguni.

Walipokuwa na kiu,

ukawapa maji kutoka katika jiwe.

Ukawaagiza kurizi inchi uliyokuwa umewaahidi.

16Lakini wao na babu zetu wakakuwa na kiburi

na wakakuwa wagumu

wakakataa kufuata maagizo yako.

17Wakakataa kutii;

hawakukumbuka maajabu uliyofanya kati yao.

Wakakuwa wagumu,

wakajichagulia kiongozi wa kuwarudisha

katika utumwa katika inchi ya Misri.

Lakini wewe Mungu uko mwepesi kwa kusamehe,

mwenye huruma na rehema,

haukasiriki upesi,

uko mwema sana.

Haukuwatupilia

18hata walipojitengenezea sanamu ya mwana-ngombe na kusema:

“Huyu ndiye Mungu wetu

aliyetutoa kutoka katika inchi ya Misri.”

Wakakuchukiza sana

19lakini wewe

kwa rehema zako nyingi

haukuwatupilia kule katika jangwa.

Nguzo la wingu lililowaongoza muchana,

wala nguzo la moto lililowaangazia katika njia usiku,

havikuondoka.

20Ukawapa Roho wako mwema kuwashauria;

ukawapa mana kuwa chakula chao,

na maji ya kunywa kwa kutuliza kiu chao.

21Ukawatunza katika jangwa kwa miaka makumi ine

na hawakukosa kitu chochote;

nguo zao hazikuchakaa

wala miguu yao haikuvimba.

22Ukawapatia ushindi juu ya falme na mataifa,

ukawafanyia mengi kila upande.

Wakashinda inchi ya Hesiboni

iliyotawaliwa na mufalme Sihoni;

na tena wakashinda inchi ya Basani

iliyotawaliwa na mufalme Ogi.

23Ukafanya wazao wao kuwa wengi

kama nyota za mbinguni;

ukawaleta katika inchi

uliyowaahidi babu zao.

24Hivyo, hao wazao wakakuja na kurizi inchi.

Ulishinda Wakanana na kuwatia katika mikono yao.

Watu wako waliweza kuwatendea vile walivyotaka

wafalme na watu wa inchi hiyo.

25Wakateka miji yenye kuta,

wakatwaa inchi yenye utajiri,

nyumba zenye vitu vingi vizuri,

visima vilivyochimbwa,

mashamba ya mizabibu na mizeituni

pamoja na miti yenye matunda kwa wingi.

Hivyo wakakula,

wakashiba na kunenepa

na kufurahia wema wako.

26Lakini hawakukuwa waaminifu kwako.

Wakakuasi,

wakaacha sheria yako

na kuwaua manabii waliowaonya

kusudi wakurudilie wewe.

Wakatenda zambi kubwa mbele yako.

27Hivyo, ukawatia katika mikono

ya waadui zao,

nao wakawatesa.

Lakini wakiwa katika mateso yao,

wakakulilia, nawe ukawasikiliza kutoka mbinguni.

Na kwa rehema zako nyingi,

ukawatumia viongozi wa kuwaokoa;

nao wakawakomboa toka katika mikono yao.

28Lakini amani ilipopatikana

wakatenda zambi tena mbele yako,

nawe ukawaacha watiwe katika mikono

ya waadui zao wawatawale.

Hata hivyo, walipotubu na kukulilia

ukawasikiliza kutoka mbinguni.

Na kwa kulingana na rehema zako nyingi,

ukawaokoa mara nyingi.

29Ukawaonya kusudi warudilie Sheria yako,

hata hivyo, kwa kiburi chao,

wakaacha kutii amri zako.

Wakaasi maagizo yako,

ambayo kwa njia yake mutu akiyatii, ataishi.

Wakakuwa wenye kiburi

vilevile wakakuwa wagumu,

na wakakataa kuwa watiifu.

30Ukawavumilia kwa miaka mingi,

na kuwaonya kwa njia ya roho wako

kwa kupitia manabii wako;

hata hivyo hawakusikiliza.

Basi ukawaacha

ukawatia katika mikono ya mataifa mengine.

31Hata hivyo,

kutokana na rehema zako nyingi,

haukuwaachilia waangamie kabisa au kuwatupilia,

maana wewe ni Mungu mwenye huruma na rehema.

32Kwa hiyo, ee Mungu wetu,

Mungu mukubwa,

mwenye nguvu na wa kutisha,

wewe unashika agano lako

na kutenda wema.

Mateso yaliyotupata, sisi,

wafalme wetu, wakubwa wetu,

makuhani wetu, manabii wetu,

babu zetu na watu wako wote

tangu wakati wa wafalme wa Asuria

mpaka leo,

usiyaone kuwa ni madogo.

33Hata hivyo,

una haki kwa kutuazibu hivyo;

maana wewe umekuwa mwaminifu

wakati sisi tumekuwa watenda maovu.

34Wafalme wetu, wakubwa wetu,

makuhani wetu na babu zetu

hawakushika Sheria yako

wala kujali amri zako

na maonyo yako uliyowapa.

35Hawakukutumikia katika ufalme wao,

wala walipofurahia mema yako mengi uliyowajalia kwa wingi,

katika inchi kubwa na yenye mboleo uliyowapa

hawakuyaacha matendo yao maovu.

36Na leo tumekuwa watumwa;

tuko watumwa katika inchi uliyowapa

babu zetu kwa kufurahia matunda yake

na mazao yake mema.

37Kwa sababu ya zambi zetu,

utajiri wa inchi hii

unawaendea wafalme uliowaleta kwa kututawala.

Wanatutawala jinsi wanavyopenda

hata na nyama wetu wa ufugo

wanawatendea jinsi wanavyopenda,

tuko katika taabu kubwa sana.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help