1Siku ya makumi mbili na ine ya mwezi ule wa saba, watu wa Israeli wakakusanyika, wakifunga kula na kuvaa nguo za magunia na kujipakaa udongo juu ya kichwa kwa kuonyesha majuto juu ya zambi zao.
2Wakati ule, walikuwa wamejitenga mbali na watu wa mataifa mengine, wakasimama na kuungama zambi zao na maovu ya babu zao.
3Kwa muda wa yapata saa tatu, walisimama wakati Sheria ya Yawe, Mungu wao, ikisomwa. Na kwa saa tatu zilizofuata, walikuwa wakitubu na kumwabudu Yawe, Mungu wao.
4Kuliwekwa daraja la Walawi; pale kulisimama Yesua, Bani, Kadimieli, Sebania, Buni, Serebia, Bani na Kenani. Wakamwomba kwa sauti kubwa Yawe, Mungu wao.
5Walawi, ni kusema Yesua, Kadimieli, Bani, Hasabuea, Serebia, Hodia, Sebania na Petahia, wakawaambia watu: Musimame na kumusifu Yawe, Mungu wenu.
Mumusifu milele na milele!
Na watu wakasifu jina lako tukufu,
ambalo linatukuka kuliko baraka na sifa zote.
Maombi ya usamehe wa zambi6Ezra akaomba akisema:
Wewe peke yako ndiwe Yawe!
Ulifanya mbingu na jeshi lake lote,
dunia na vyote vinavyokuwa ndani yake,
bahari na vyote vinavyokuwa ndani yake.
Unavipatia uzima,
na jeshi lote la mbinguni linakuabudu wewe.
7Wewe ndiwe Yawe,
Mungu uliyemuchagua Abramu.
Ukamutoa toka Uri ya Wakaldea
na kumupa jina la Abrahamu.
8Ukamwona kuwa wa haki mbele yako;
ukafanya agano naye kuwapa wazao wake inchi ya Wakanana,
Wahiti, Waamori, Waperizi, Wayebusi na Wagirgasi.
Na ahadi yako ukaitimiza;
maana wewe ni mwaminifu.
9Uliyaona mateso ya babu zetu
walipokuwa katika inchi ya Misri,
na walipokuomba musaada kwenye bahari Nyekundu
ukawasikiliza.
10Ulifanya miujiza na maajabu mbele ya Mufalme wa Misri,
watumishi wake wote
na watu wote wa inchi yake;
maana ulijua kwamba
waliwagandamiza babu zetu.
Ukajipatia utukufu unaokuwa mpaka leo.
11Uligawanya bahari katikati mbele yao,
nao wakapita katikati ya bahari,
pahali pakavu.
Lakini ukawatupa Wamisri
waliowafuatilia kama jiwe zito
ndani ya maji mengi.
12Muchana uliwaongoza kwa nguzo la wingu,
na usiku uliwaongoza kwa nguzo la moto
kwa kuwaangazia njia ya kufuata.
13Kule kwa mulima Sinai
ulishuka toka mbinguni na kuzungumuza nao.
Ukawapa maagizo safi, sheria za kweli,
masharti mazuri na amri.
14Kwa njia ya Musa, mutumishi wako,
ukawajulisha siku zako za Sabato takatifu
na ukawaagiza kuzifuata amri,
masharti na sheria ulizowaamuru.
15Walipokuwa na njaa,
ukawapa chakula kutoka mbinguni.
Walipokuwa na kiu,
ukawapa maji kutoka katika jiwe.
Ukawaagiza kurizi inchi uliyokuwa umewaahidi.
16Lakini wao na babu zetu wakakuwa na kiburi
na wakakuwa wagumu
wakakataa kufuata maagizo yako.
17Wakakataa kutii;
hawakukumbuka maajabu uliyofanya kati yao.
Wakakuwa wagumu,
wakajichagulia kiongozi wa kuwarudisha
katika utumwa katika inchi ya Misri.
Lakini wewe Mungu uko mwepesi kwa kusamehe,
mwenye huruma na rehema,
haukasiriki upesi,
uko mwema sana.
Haukuwatupilia
18hata walipojitengenezea sanamu ya mwana-ngombe na kusema:
“Huyu ndiye Mungu wetu
aliyetutoa kutoka katika inchi ya Misri.”
Wakakuchukiza sana
19lakini wewe
kwa rehema zako nyingi
haukuwatupilia kule katika jangwa.
Nguzo la wingu lililowaongoza muchana,
wala nguzo la moto lililowaangazia katika njia usiku,
havikuondoka.
20Ukawapa Roho wako mwema kuwashauria;
ukawapa mana kuwa chakula chao,
na maji ya kunywa kwa kutuliza kiu chao.
21Ukawatunza katika jangwa kwa miaka makumi ine
na hawakukosa kitu chochote;
nguo zao hazikuchakaa
wala miguu yao haikuvimba.
22Ukawapatia ushindi juu ya falme na mataifa,
ukawafanyia mengi kila upande.
Wakashinda inchi ya Hesiboni
iliyotawaliwa na mufalme Sihoni;
na tena wakashinda inchi ya Basani
iliyotawaliwa na mufalme Ogi.
23Ukafanya wazao wao kuwa wengi
kama nyota za mbinguni;
ukawaleta katika inchi
uliyowaahidi babu zao.
24Hivyo, hao wazao wakakuja na kurizi inchi.
Ulishinda Wakanana na kuwatia katika mikono yao.
Watu wako waliweza kuwatendea vile walivyotaka
wafalme na watu wa inchi hiyo.
25Wakateka miji yenye kuta,
wakatwaa inchi yenye utajiri,
nyumba zenye vitu vingi vizuri,
visima vilivyochimbwa,
mashamba ya mizabibu na mizeituni
pamoja na miti yenye matunda kwa wingi.
Hivyo wakakula,
wakashiba na kunenepa
na kufurahia wema wako.
26Lakini hawakukuwa waaminifu kwako.
Wakakuasi,
wakaacha sheria yako
na kuwaua manabii waliowaonya
kusudi wakurudilie wewe.
Wakatenda zambi kubwa mbele yako.
27Hivyo, ukawatia katika mikono
ya waadui zao,
nao wakawatesa.
Lakini wakiwa katika mateso yao,
wakakulilia, nawe ukawasikiliza kutoka mbinguni.
Na kwa rehema zako nyingi,
ukawatumia viongozi wa kuwaokoa;
nao wakawakomboa toka katika mikono yao.
28Lakini amani ilipopatikana
wakatenda zambi tena mbele yako,
nawe ukawaacha watiwe katika mikono
ya waadui zao wawatawale.
Hata hivyo, walipotubu na kukulilia
ukawasikiliza kutoka mbinguni.
Na kwa kulingana na rehema zako nyingi,
ukawaokoa mara nyingi.
29Ukawaonya kusudi warudilie Sheria yako,
hata hivyo, kwa kiburi chao,
wakaacha kutii amri zako.
Wakaasi maagizo yako,
ambayo kwa njia yake mutu akiyatii, ataishi.
Wakakuwa wenye kiburi
vilevile wakakuwa wagumu,
na wakakataa kuwa watiifu.
30Ukawavumilia kwa miaka mingi,
na kuwaonya kwa njia ya roho wako
kwa kupitia manabii wako;
hata hivyo hawakusikiliza.
Basi ukawaacha
ukawatia katika mikono ya mataifa mengine.
31Hata hivyo,
kutokana na rehema zako nyingi,
haukuwaachilia waangamie kabisa au kuwatupilia,
maana wewe ni Mungu mwenye huruma na rehema.
32Kwa hiyo, ee Mungu wetu,
Mungu mukubwa,
mwenye nguvu na wa kutisha,
wewe unashika agano lako
na kutenda wema.
Mateso yaliyotupata, sisi,
wafalme wetu, wakubwa wetu,
makuhani wetu, manabii wetu,
babu zetu na watu wako wote
tangu wakati wa wafalme wa Asuria
mpaka leo,
usiyaone kuwa ni madogo.
33Hata hivyo,
una haki kwa kutuazibu hivyo;
maana wewe umekuwa mwaminifu
wakati sisi tumekuwa watenda maovu.
34Wafalme wetu, wakubwa wetu,
makuhani wetu na babu zetu
hawakushika Sheria yako
wala kujali amri zako
na maonyo yako uliyowapa.
35Hawakukutumikia katika ufalme wao,
wala walipofurahia mema yako mengi uliyowajalia kwa wingi,
katika inchi kubwa na yenye mboleo uliyowapa
hawakuyaacha matendo yao maovu.
36Na leo tumekuwa watumwa;
tuko watumwa katika inchi uliyowapa
babu zetu kwa kufurahia matunda yake
na mazao yake mema.
37Kwa sababu ya zambi zetu,
utajiri wa inchi hii
unawaendea wafalme uliowaleta kwa kututawala.
Wanatutawala jinsi wanavyopenda
hata na nyama wetu wa ufugo
wanawatendea jinsi wanavyopenda,
tuko katika taabu kubwa sana.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.