1Kutakuja wakati ambapo
mulima wa nyumba ya Yawe
utakuwa mukubwa kuliko milima yote.
Utanyanyuliwa juu ya vilima vyote.
Watu wengi watakimbilia kule,
2mataifa mengi yataufikia na kusema:
Tuende juu kwenye mulima wa Yawe,
tuende katika nyumba ya Mungu wa Yakobo,
kusudi atufundishe njia zake,
nasi tuzifuate.
Maana sheria itatoka kule Sayuni;
na neno la Yawe kule Yerusalema.
3Mungu atatoa hukumu kati ya mataifa mengi,
atakata mashauri ya mataifa makubwa ya mbali.
Nayo yatafua mapanga yao kuwa majembe,
na mikuki yao kuwa visu vya kuvuna.
Taifa halitapigana na taifa lingine,
wala hayatafanya tena mazoezi ya vita.
4Kila mutu atakaa kwa amani
chini ya miti ya tini na mizabibu yake,
bila kutishwa na mutu yeyote.
–Maneno haya yanatoka katika kinywa cha Yawe wa majeshi.
5Mataifa mengine yanafuata njia zao,
kwa kuitegemea miungu yao,
lakini sisi tunafuata njia zetu kwa kumutegemea Yawe,
Mungu wetu, milele na milele.
Waisraeli watarudi kutoka katika utumwa6Siku ile,
nitawakusanya waliolemewa,
nitawakusanya waliopelekwa katika uhamisho,
watu wale ambao niliwaazibu.
–Ni ujumbe wa Yawe.–
7Hao waliolemewa ndio watakaobaki wazima;
hao waliopelekwa katika uhamisho watakuwa taifa lenye nguvu.
Yawe atawatawala kwenye mulima Sayuni,
tangu wakati ule na hata milele.
8Nawe kilima cha Yerusalema,
wewe munara wa Sayuni,
ambamo Mungu anafanya ulinzi juu ya watu wake,
kama muchungaji juu ya kondoo wake,
wewe utakuwa tena muji wenye mamlaka sawa zamani.
Yerusalema utakuwa tena muji mukubwa wa mufalme.
9Sasa kwa nini munalia kwa sauti?
Hamuna mufalme tena?
Mushauri wenu ametoweka?
Munalalamika kwa uchungu,
kama mwanamuke anayezaa!
10Enyi watu wa Sayuni,
mulie na kugaagaa kama mwanamuke anayezaa!
Maana sasa mutaondoka katika muji huu
muende kukaa katika mbuga,
mutakwenda mpaka Babeli.
Lakini kule, mutaokolewa.
Kule Yawe atawakomboa toka katika makucha ya waadui zenu.
11Mataifa mengi yamekusanyika kwa kuwashambulia.
Yanasema: Muache muji wao uchafuliwe,
nasi tufurahie kuona uharibifu wa Sayuni!
12Lakini wao
hawafahamu mawazo ya Yawe
wala hawaelewi mupango wake:
kwamba amewakusanya pamoja,
kama miganda pahali pa kupepetea.
13Yawe anasema:
Enyi watu wa Sayuni,
musimame muwakanyagekanyage!
Nitawapatia nguvu kama ngombe dume
mwenye pembe za chuma na kwato za shaba.
Mutawasaga watu wa mataifa mengi;
mutanitolea mimi mapato yao,
mutanitolea mali zao mimi Bwana wa dunia yote.
14Mujikusanye enyi watu wa Yerusalema;
mukisema: Tumeshambuliwa, tumesongwa;
naye mutawala wa Israeli wanamupiga fimbo kwenye shavu.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.