1Katika mwaka wa kumi na saba wa utawala wa Peka mwana wa Remalia, mufalme wa Israeli, Ahazi mwana wa Yotamu, mufalme wa Yuda, akaanza kutawala.
2Alikuwa na umri wa miaka makumi mbili alipoanza kutawala. Akatawala kwa muda wa miaka kumi na sita akiwa kule Yerusalema. Hakutenda kwa usawa mbele ya Yawe kama vile Daudi babu yake alivyofanya,
3lakini alifuata mwenendo wa wafalme wa Israeli. Akamutambikia hata mwana wake kwa kuteketezwa kwa moto, akifuata desturi mbaya za mataifa ambayo yalifukuzwa na Yawe wakati Waisraeli walipokuwa wanaingia katika inchi.
4Ahazi alitambikia sadaka na kufukiza ubani kwenye nafasi yenye kuinuka, juu ya vilima na chini ya kila muti wenye majani mengi.
5Kisha Resini mufalme wa Aramu na Peka mwana wa Remalia mufalme wa Israeli walitokea kwa kupiga vita na Yerusalema, nao waliuzunguka, lakini hawakuweza kuuteka.
6Wakati ule, mufalme wa Edomu aliuteka akawarudishia Waedomu muji wa Elati na kuwafukuza watu wa Yuda waliokaa mule. Nao Waedomu wakaingia Elati na kufanya makao yao kule mpaka sasa.
7Basi Ahazi akatuma watu kwa mufalme Tigilati-Pileseri wa Asuria wakiwa na ujumbe huu: “Mimi ni mutumishi wako mwaminifu. Ukuje uniokoe kutoka kwa wafalme wa Aramu na Israeli ambao wananishambulia.”
8Ahazi akatwaa feza na zahabu iliyokuwa katika nyumba ya Yawe na hazina iliyokuwa katika nyumba ya mufalme na kumupelekea kama zawadi mufalme wa Asuria.
9Tigilati-Pileseri, akiitika kwa ombi la Ahazi, aliushambulia muji wa Damasiki na kuuteka. Akamwua mufalme Resini na kuwapeleka wafungwa kule Kiri.
10Mufalme Ahazi alipokwenda Damasiki kukutana na mufalme Tigilati-Pileseri, aliona mazabahu kule. Basi, akamutumia kuhani Uria mufano kamili na muchoro wa mazabahu hiyo.
11Uria akajenga mazabahu ile kulingana na mufano ule na kuimaliza mbele ya kurudi kwa Ahazi.
12Ahazi aliporudi kutoka Damasiki, aliiona mazabahu ile; basi akaikaribia mazabahu na kutoa sadaka juu yake.
13Alitolea sadaka yake ya kuteketezwa, ya ngano, na ya kinywaji, akanyunyiza damu ya sadaka ya amani.
14Mazabahu ya shaba ambayo ilitakaswa kwa ajili ya Yawe, aliiondoa mbele ya nyumba kutoka nafasi yake katikati ya mazabahu yake na nyumba ya Yawe, akaiweka kwenye nafasi iliyokuwa upande wa kaskazini wa mazabahu yake.
15Kisha alimwamuru Uria: “Tumia hii mazabahu yangu kubwa kwa kuteketeza sadaka za asubui na sadaka za unga za magaribi, sadaka za kuteketezwa, sadaka za unga za mufalme na za watu wote na vilevile sadaka za divai za watu. Unyunyize damu ya nyama wote wa kuteketezwa ambao wametolewa sadaka. Lakini ile mazabahu ya shaba nitaitumia mimi kwa kuuliza shauri toka kwa Mungu.”
16Naye Uria akafuata maagizo ya mufalme.
17Mufalme Ahazi aliviondoa vile vishikio vilivyokuwa vikisimamishwa kule, akaondoa na bakuli lake ambalo lilikuwa juu ya wale ngombe dume kumi na wawili wa shaba na kuliweka juu ya musingi wa mawe.
18Nalo baraza la Sabato lililokuwa limejengwa ndani ya nyumba pamoja na mulango wa inje, mufalme alivihamisha kutoka katika nyumba ya Yawe kwa ajili ya mufalme wa Aramu.
19Matendo mengine yote ya mufalme Ahazi yameandikwa katika Kitabu cha Mambo ya Siku za Wafalme wa Yuda.
20Ahazi akakufa na kuzikwa katika makaburi ya kifalme katika muji wa Daudi, naye mwana wake Hezekia akatawala kwa pahali pake.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.