1Nimeona jambo moja ovu hapa chini ya jua, linalowagandamiza watu:
2Mungu anamujalia mutu utajiri, mali na heshima, hata hakosewi kitu chochote anachotamani, lakini hamupi uwezo wa kuvifurahia vitu hivyo. Pahali pake, mugeni fulani atavifaidia. Hayo nayo ni bure. Ni jambo la mateso mabaya.
3Mutu akiweza kuzaa watoto mia moja, na akiishi maisha marefu, lakini kama mutu huyo hafurahii maisha yake, wala hafanyiwi mazishi, basi ninasema mutoto aliyezaliwa amekufa ni afazali kuliko mutu yule.
4Mutoto mufu anakuja kwa bure naye anarudi katika giza, na kusahaulika.
5Zaidi ya hayo, mutoto wa namna hiyo hakupata kuuona mwangaza wa jua wala kutambua kitu chochote. Hata hivyo, yule mutoto anapumzika kuliko yule mutu.
6Ingawa mutu huyo ataishi miaka elfu mbili, lakini hafurahii maisha, basi yeye ni kama yule mutoto. Wote wawili wanakwenda fasi moja.
7Mutu anatoa jasho kwa ajili ya kupata chakula, lakini tamaa yake ya kula haitoshelezwi hata kidogo.
8Basi mutu mwenye hekima ana faida zaidi kuliko mupumbafu? Na mutu masikini anapata faida gani akijua namna ya kuishi?
9Hayo nayo ni bure sawa na kutaka kumata upepo. Afazali kufurahia kitu ambacho uko nacho kuliko kuhangaika kwa kutamani kitu kingine.
10Kila kitu kinachotukia kilikwisha kupangwa tangu zamani. Hali ya mwanadamu inajulikana, na tunajua kwamba muzaifu hawezi kubishana na mutu mwenye nguvu zaidi.
11Maneno yanapokuwa mengi, ndivyo yanaendelea kuwa bure. Hayana faida.
12Nani anayejua yanayofaa kwa mutu katika maisha haya mafupi yasiyokuwa na faida, maisha ambayo yanapita kama kivuli? Nani anayejua yale yatakayotukia chini ya jua nyuma ya kufa kwake?
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.