1Mufuate mufano wangu kama vile mimi ninavyofuata mufano wa Kristo.
Mavalio ya mwanamuke wakati wa ibada2Ninawashukuru kwa sababu munanikumbuka katika mambo yote na kwa sababu munashika mafundisho yangu sawa vile nilivyoyafundisha kwenu.
3Lakini ninataka mufahamu maneno haya: Kristo ni kichwa cha kila mwanaume, na mwanaume ni kichwa cha muke wake, na Mungu ni kichwa cha Kristo.
4Basi mwanaume yeyote akifunika kichwa chake wakati anapoomba Mungu, au anapotabiri, anamuzaraulisha Kristo.
5Lakini mwanamuke yeyote asipofunika kichwa chake wakati anapoomba au anapotabiri, anamuzaraulisha mume wake. Tendo hilo linahesabiwa kama vile amenyolewa.
6Kama mwanamuke hafuniki kichwa, anaweza basi kunyolewa! Lakini kwa sababu ni haya kwa mwanamuke kukatwa nywele au kunyolewa, basi inafaa afunike kichwa.
7Mwanaume hapaswi kufunika kichwa, kwa sababu yeye ni mufano na utukufu wa Mungu. Lakini mwanamuke ni utukufu wa mwanaume.
8Kwa maana mwanaume hakuumbwa kutoka katika mwanamuke, lakini mwanamuke aliumbwa kutoka katika mwanaume.
9Na zaidi ya hii, mwanaume hakuumbwa kwa ajili ya mwanamuke, lakini mwanamuke aliumbwa kwa ajili ya mwanaume.
10Kwa hiyo, kwa sababu ya wamalaika, mwanamuke anapaswa kufunika kichwa chake kuwa kitambulisho kinachoonyesha kuwa yuko chini ya mamlaka ya mume wake.
11Lakini katika ushirika wetu na Bwana, hakuwezi kuwa mwanamuke pasipo mwanaume wala mwanaume pasipo mwanamuke.
12Kwa maana kama vile mwanamuke alivyoumbwa kutoka katika mwanaume, vilevile mwanaume anazaliwa na mwanamuke; na vyote vinatoka kwa Mungu.
13Muamue ninyi wenyewe: ni vema mwanamuke asifunike kichwa anapoomba Mungu wakati wa ibada?
14Hali ya asili yenyewe inawaonyesha kuwa ni haya kwa mwanaume kuwa na nywele ndefu,
15lakini ni heshima kwa mwanamuke kuwa na nywele ndefu. Kwa maana nywele ndefu zimetolewa kwa mwanamuke kwa kuwa nguo ya kufunika kichwa.
16Lakini kama mutu akitaka kubishana juu ya neno hili, ajue kwamba sisi wala makanisa ya Mungu hatuna desturi ingine.
Ukumbusho wa karamu ya Bwana(Mat 26.26-29; Mk 14.22-25; Lk 22.15-20)17Kuelekea maonyo yanayofuata, mimi siwasifu. Kwa maana munapokusanyika, mikutano yenu haiwafalii, lakini inawaletea hasara.
18Kwanza, ninasikia kwamba munapokusanyika kuna matengano katikati yenu, nami ninasadiki kwamba nusu ya maneno yale ni ya kweli.
19(Inafaa kuwe matengano kati yenu, kusudi wale wanaokuwa waaminifu wa kweli kati yenu wajulikane.)
20Munapokusanyika hamukuli karamu ya Bwana.
21Kwa maana munapokula, kila mumoja anajiharikisha kula chakula chake mwenyewe, hivi wamoja wenu wanasikia njaa na wengine wanalewa.
22Basi, ninyi hamuna nyumba munamoweza kukulia na kukunywea? Au munazarau kanisa la Mungu na munataka kuwapatisha haya wale wasiokuwa na kitu? Munataka niwaambie ninyi nini? Inafaa niwasifu? Hapana, siwezi kuwasifu hata kidogo juu ya jambo hilo!
23Kwa maana haya ndiyo mafundisho niliyopokea kutoka kwa Bwana, nami niliyotoa kwenu: katika usiku ule Bwana Yesu alipotolewa, alitwaa mukate,
24na alipokwisha kumushukuru Mungu, akaumega akisema: “Huu ni mwili wangu unaotolewa kwa ajili yenu. Mufanye hivi kwa kunikumbuka.”
25Vilevile, nyuma ya kula akatwaa kikombe na kusema: “Kikombe hiki ni agano jipya la Mungu, linalohakikishwa kwa njia ya damu yangu. Mufanye hivi kwa kunikumbuka kila mara munapokikunywa.”
26Kwa sababu kila mara munapokula mukate huu na kunywa kikombe hiki, munatangaza kufa kwa Bwana mpaka atakapokuja.
27Basi kila mutu anayekula mukate wa Bwana au kunywa kikombe chake bila kustahili, anafanya zambi akikosea mwili na damu ya Bwana.
28Basi kila mutu ajichunguze mwenyewe na kisha akule mukate huu na kunywa kikombe hiki.
29Kwa maana mutu akikula mukate na kunywa kikombe pasipo kutambua maana ya mwili wa Bwana, anajiletea azabu yeye mwenyewe kwa kula na kunywa.
30Na kwa sababu hii wengi kati yenu ni wagonjwa na wazaifu, na wengi wamekufa.
31Lakini tungejichunguza sisi wenyewe kwanza, hatungehukumiwa na Mungu.
32Lakini tunahukumiwa na kuazibiwa na Bwana kusudi tusiazibiwe pamoja na watu wa dunia hii.
33Kwa hiyo wandugu zangu, wakati munapokusanyika kwa kula karamu ya Bwana, sherti mungojeane.
34Kama mutu akiwa na njaa, akule katika nyumba yake, kusudi musikusanyike kwa kujiletea azabu.
Basi maneno mengine yanayobaki nitayatengeneza wakati nitakapofika kwenu.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.