Mezali 22 - Swahili Congo Revised Bible 2002

1Afazali kuwa na sifa nzuri kuliko mali mengi. Kupata kukubaliwa ni bora kuliko feza au zahabu.

2Watajiri na wamasikini wana hali hii moja: Yawe ni Muumba wao wote.

3Mwenye akili anaona hatari na kujificha, lakini wajinga wanajitokeza mbele na kuumia.

4Ukinyenyekea na kumwogopa Yawe, utapata zawadi ya fanaka, heshima, na uzima.

5Njia ya waovu imejaa miiba na mitego; anayetaka kulinda maisha yake ataiepuka.

6Umufundishe mutoto njia anayopaswa kufuata, naye hataiacha hata katika uzee.

7Tajiri anamutawala masikini. Mwenye kukopesha ni mutumwa wa mwenye kukopeshwa.

8Anayepanda ubaya atavuna hasara. Uwezo wake wa kutenda mabaya utavunjwa.

9Mutu mwenye kuwa tayari kusaidia atabarikiwa, maana anagawanya chakula chake na masikini.

10Umufukuze mwenye kiburi na fujo itatoweka, na ugomvi na matusi vitakoma.

11Mwenye nia safi na maneno mazuri atakuwa rafiki wa mufalme.

12Yawe analinda maarifa lakini anayavuruga maneno ya waovu.

13Muvivu anasema: “Kuna simba inje. Nitauawa katika njia.”

14Kinywa cha mwasherati ni shimo refu; anayechukiwa na Yawe atatumbukia ndani yake.

15Ujinga umefungwa ndani ya moyo wa mutoto, lakini fimbo ya kufundisha itaufukuza mbali.

16Anayemutesa masikini kwa kujitajirisha na anayewapa watajiri zawadi, wote wawili wataishia kuwa wamasikini.

Misemo ya wenye hekima

17Tega sikio usikie maneno ya wenye hekima;

elekeza moyo wako kwa maarifa yangu.

18Wewe utafurahi kama utayaweka ndani ya moyo,

na kuyarudiliarudilia kila wakati.

19Ninayependa kumufundisha leo ni wewe,

kusudi tumaini lako likuwe kwa Yawe.

20Nimekuandikia misemo makumi tatu,

misemo ya maonyo na maarifa,

21kwa kukufundisha mambo yanayokuwa sawa na kweli;

na mutu akikuuliza upate kumupa jibu la kweli.

22Usinyanganye masikini mali yake kwa sababu ni masikini,

wala usimunyime mukosefu haki yake katika tribinali.

23Maana Yawe atawatetea;

atagandamiza maisha ya wale wanaowagandamiza.

24Usifanye urafiki na mutu wa hasira,

wala usiandamane na mwenye kukasirika upesi.

25Usijifunze mwenendo wake,

na kujinasa kabisa katika mutego.

26Usikuwe mumoja wa wale ambao wanajitoa rehani kwa madeni ya wengine.

27Ikiwa hauna chochote cha kulipa,

hata kitanda unacholalia kitanyanganywa!

28Usiondoe kitambulisho cha mupaka wa zamani,

ambacho kiliwekwa na babu zako.

29Kuna mutu mwenye akili na maarifa ndani ya kazi?

Yule atawatumikia wafalme;

hatawatumikia watu wasiofaa.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help