1Mungu aliniambia niimbe wimbo huu wa maombolezo juu ya wakubwa wa Waisraeli:
2Mama yenu alikuwa simba mwenye utukufu
kati ya simba wengine.
Alikaa kati ya simba wakali,
akawalisha watoto wake.
3Alimulea mutoto mumoja kati ya watoto wake,
mutoto huyo naye akakuwa simba mukali.
Akajifunza toka kwa mama yake kuwinda,
akakuwa simba mukula watu.
4Mataifa yakatangaza habari ya hatari juu yake,
wakamunasa katika mutego wao,
wakamupeleka juu ya ndoana mpaka Misri.
5Mama yake alipoona kwamba amechoka kungoja,
matumaini ya kumupata yakakwisha,
akamutwaa mutoto wake mwingine,
akamufanya simba mukali.
6Huyo alipokuwa amekwisha kukomaa,
akaanza kutembea pamoja na simba wengine.
Naye vilevile akajifunza kuwinda,
akakuwa simba mukula watu.
7Alishambulia nyumba za watu
na kuiharibu miji yao.
Inchi pamoja na wakaaji wake viliogopa,
kwa sauti ya kunguruma kwake.
8Mataifa yakamushambulia kutoka pande zote,
wakatandaza wavu wao juu yake,
naye akanaswa katika mutego wao.
9Kwa ndoana wakamutia katika kizimba chao,
wakamupeleka kwa mufalme wa Babeli.
Kule, wakamutia katika kifungo,
kusudi ngurumo yake isisikilike tena
juu ya milima ya Waisraeli.
10Mama yako alikuwa kama muzabibu katika shamba,
uliopandikizwa pembeni ya maji,
ambao ulizaa sana kwa kuwa na maji mengi.
11Ulikuwa na matawi yenye nguvu,
ambayo yalikuwa fimbo za kifalme.
Muzabibu huo ulikomaa kupita miti mingine,
watu walisifu ukubwa wa shina lake
na wingi wa matawi yake.
12Lakini uliongolewa kwa hasira,
ukatupwa chini juu ya udongo;
upepo mukali wa mashariki ukaukausha,
matunda yake yakaanguka;
matawi yake yenye nguvu yalikauka,
nao moto ukauteketeza.
13Na sasa umepandikizwa katika jangwa,
katika inchi yenye kukauka isiyokuwa na maji.
14Lakini moto umetoka kwenye shina lake,
ukayateketeza matawi na matunda yake.
Matawi yake hayatakuwa na nguvu hata kidogo,
wala hayatakuwa fimbo za kifalme.
Huo umekuwa wimbo wa maombolezo; ndivyo unavyoimbwa siku zote.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.