1Mimi ninataka kusema hivi: mwana anayepaswa kurizi mali ya baba yake anatendewa kama mutumwa kwa muda wote anapokuwa angali mudogo, ijapokuwa yeye ndiye kweli mwenyeji wa mali yote.
2Kwa muda ule yeye ni chini ya madaraka ya watu wanaomuchunga na ya walinzi wa mali mpaka wakati baba yake aliopanga upate kutimia.
3Na sisi vilevile tulipokuwa tungali kama watoto, tulikuwa watumwa wa vitu vyenye uwezo vilivyotawala dunia.
4Lakini wakati uliopangwa ulipotimia, Mungu akamutuma Mwana wake: akazaliwa na mwanamuke na kuishi chini ya uongozi wa Sheria,
5kusudi awakomboe wale walioishi chini ya uongozi wa Sheria. Alifanya vile kusudi tupate kuwa wana wa Mungu.
6Mungu alituma Roho wa Mwana wake ndani ya moyo wetu kwa kuhakikisha ya kuwa ninyi ni wana wake. Roho anayetuombea, akiita: “Baba!”
7Basi wewe si mutumwa tena, lakini mwana, na kwa kuwa wewe ni mwana wake, Mungu atakupa sehemu ya urizi aliouahidi kwa wana wake.
Wasiwasi wa Paulo juu ya Wagalatia8Zamani, mulipokuwa hamumujui Mungu, mulikuwa watumwa wa miungu isiyokuwa ya kweli.
9Lakini sasa munamujua Mungu, au afazali tuseme kwamba sasa munajulikana naye. Basi namna gani mumerudilia tena vitu vinavyotawala dunia, visivyokuwa na uwezo na vikosefu, mukitaka kuwa watumwa tena?
10Kwa nini munashugulika na kutimiza desturi zenu za siku, miezi, nyakati na za miaka?
11Ninawaogopea, kwa maana inawezekana kwamba nimesumbuka bure kwa ajili yenu!
12Wandugu zangu, ninawasihi mukuwe kama mimi, kwa kuwa mimi nimekuwa kama ninyi. Ninyi hamukunitendea ubaya wowote.
13Munakumbuka kwamba niliwahubiri Habari Njema kwa mara ya kwanza kwa sababu ya ugonjwa nilioupata.
14Mulipata majaribu kwa sababu ya hali ya mwili wangu. Ingawa hivi hamukunizarau wala kuchukizwa nami, lakini mulinipokea sawa vile mungepokea malaika wa Mungu au Yesu Kristo!
15Ninyi mulikuwa wenye furaha. Sasa nini imewatokea? Kwa maana ninaweza kuwashuhudia kwamba mungeweza kuongoa hata macho yenu na kuyatoa kwangu!
16Basi nimegeuka sasa adui yenu kwa sababu ya kuwaambia ukweli?
17Wale watu wanaonyesha kwamba wanawashugulikia, lakini nia yao si nzuri. Wao wanataka kuwatenganisha na mimi, kusudi mupate kushugulika nao.
18Ni vizuri kushugulika na mambo mema siku zote, wala si wakati ninapokuwa pamoja nanyi tu.
19Watoto wangu wapendwa, kama vile mwanamuke anavyopata uchungu wa kuzaa, mimi vilevile, ninapata tena uchungu kwa ajili yenu mpaka mutakapokuwa na hali inayokuwa kama ya Kristo ndani yenu.
20Ningependa kuwa pamoja nanyi sasa, kwa maana ningetumia usemi mwingine. Ninashikwa na wasiwasi kwa ajili yenu.
Mufano wa Hagari na Sara21Muniambie ninyi munaotaka kuishi chini ya Sheria, hamujui vile Sheria inavyosema?
22Imeandikwa kwamba Abrahamu alikuwa na wana wawili. Alizaa mwana mumoja na muke wake mujakazi na mwingine na muke wake huru wa ndoa.
23Yule mwana wa mujakazi alizaliwa sawa kawaida, lakini yule wa muke huru alizaliwa kutokana na ahadi ya Mungu.
24Maneno haya ni kama vile mufano: wake hawa wawili ni mufano wa maagano mawili. Yule Hagari, watoto wake waliozaliwa katika hali ya utumwa, ni mufano wa agano lililofanyika kwenye mulima Sinai.
25Hagari analinganishwa na mulima Sinai wa inchi ya Arabia, na ni mufano wa Yerusalema ya sasa, unaokuwa katika utumwa pamoja na wakaaji wake.
26Lakini Yerusalema ya mbinguni ni huru, nao ni mama yetu.
27Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema:
“Ufurahi wewe tasa, ushangilie,
upige kelele wewe usiyejua uchungu wa kuzaa.
Kwa maana muke aliyeachwa na mume,
atakuwa na watoto wengi kuliko yule anayekuwa naye.”
28Nanyi wandugu ni watoto wa Mungu waliozaliwa kutokana na ahadi yake kama vile Isaka.
29Zamani mutoto aliyezaliwa sawa kawaida alimutesa yule aliyezaliwa kwa uwezo wa Roho wa Mungu, na ingali inafanyika vile hata sasa.
30Lakini Maandiko Matakatifu yanasema nini? Yanasema: “Fukuza mujakazi huyu pamoja na mwana wake; kwa maana mwana wa mujakazi hatarizi pamoja na mwana wa muke huru.”
31Hivi wandugu, sisi hatuko watoto wa mujakazi, lakini sisi ni watoto wa muke huru.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.