1 Wakorinto 15 - Swahili Congo Revised Bible 2002

1Wandugu zangu, sasa ninataka kuwakumbusha Habari Njema niliyowatangazia, ile muliyopokea na kuishika imara.

2Nanyi kwa njia ya habari hiyo munaokolewa, ikiwa munaishika kufuatana na maneno niliyowahubiri. Kama isipokuwa hivi, muliamini bure.

3Kwanza nimewatolea mafundisho haya ambayo mimi mwenyewe nilipokea: Kristo alikufa kwa sababu ya zambi zetu kama vile Maandiko Matakatifu yanavyosema.

4Alizikwa na kufufuliwa kwa siku ya tatu kisha kufa kwake kama vile Maandiko Matakatifu yanavyosema.

5Alimutokea Petro, na kisha akawatokea mitume wake kumi na wawili.

6Nyuma aliwatokea waamini zaidi ya mia tano pamoja, na wengi kati yao wangali wanaishi mpaka sasa, lakini wachache wamekwisha kufa.

7Kisha alimutokea Yakobo, na nyuma akawatokea mitume wote.

8Na kwa mwisho wa wote akanitokea mimi vilevile, mimi ninayekuwa kama mutoto aliyezaliwa pasipo kutimiza miezi.

9Kwa maana mimi ni mudogo kati ya mitume wote, nami sistahili hata kuitwa mutume, kwa maana nilitesa kanisa la Mungu.

10Lakini kwa neema ya Mungu nimekuwa sawa hivi ninavyokuwa, na neema yake niliyopewa haikukuwa ya bure, lakini nilitumika zaidi sana kuliko mitume wote wengine. Hakika si mimi, lakini ni neema ya Mungu inayokuwa pamoja nami.

11Basi, ikiwa ni mimi au ikiwa ni wao, hii ndiyo habari tunayohubiri na ndiyo muliyoamini.

Ufufuko wetu

12Ikiwa tunahubiri kuwa Kristo amefufuka, namna gani basi wengine kati yenu wanasema kama wafu hawatafufuka?

13Basi ikiwa kweli wafu hawatafufuka, Kristo vilevile hakufufuka.

14Na kama Kristo hakufufuka, mahubiri yetu ni ya bure na kuamini kwenu ni kwa bure vilevile.

15Na zaidi ya hii, sisi tumeonekana kuwa washuhuda wa uongo mbele ya Mungu, kwa sababu tumeshuhudia kuwa Mungu amemufufua Kristo, ingawa hakumufufua, ikiwa kweli wafu hawafufuki.

16Kwa maana kama wafu hawafufuki, basi Kristo naye hakufufuka.

17Na kama Kristo hakufufuka, imani yenu ni ya bure, na mungali katika zambi zenu.

18Na zaidi ya hii, wale waliokufa wakiamini Kristo wamepotea kabisa.

19Ikiwa tunamutumainia Kristo juu ya maisha haya ya sasa tu, sisi ni wamasikini kuliko watu wote.

20Lakini, kwa hakika Kristo amefufuka na hii inahakikisha kwamba wale waliokufa watafufuliwa vilevile.

21Kwa maana, kama vile kifo kililetwa na mutu mumoja, vilevile ufufuko wa wafu unaletwa na mutu mumoja.

22Kama vile watu wote wanavyokufa kwa sababu ya kuungana kwao na Adamu, vilevile wote wataishi tena kwa sababu ya kuungana kwao na Kristo.

23Lakini kila mutu atafufuka kufuatana na utaratibu wake; Kristo ndiye anayekuwa wa kwanza, na kisha watu wake watafufuka, wakati atakaporudia.

24Na nyuma ya pale, mwisho wa vyote utatimia. Wakati ule Kristo ataharibu utawala wote, mamlaka yote na uwezo wote, naye atamupatia Mungu Baba ufalme.

25Kwa maana Kristo anapaswa kutawala mpaka atakapowashinda waadui zake wote na kuwaweka chini ya miguu yake.

26Adui wa mwisho atakayeangamizwa ni kifo.

27Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Mungu aliweka vitu vyote chini ya miguu yake.” Ndiyo Maandiko Matakatifu yanasema kwamba alipewa mamlaka juu ya vitu vyote. Lakini maneno haya yanaonyesha wazi kwamba Mungu hahesabiwi katika hili neno “Vyote”, kwa maana ni yeye aliyemupa mamlaka juu ya vitu vyote.

28Na wakati vitu vyote vitakapokuwa vimewekwa chini ya mamlaka ya Mwana, halafu yeye mwenyewe atajiweka chini ya mamlaka ya Mungu aliyemupa mamlaka juu ya vitu vyote, kusudi Mungu apate kutawala juu ya vyote kabisa.

29Ikiwa hakuna ufufuko, wale wanaobatizwa kwa ajili ya wafu watafanya nini? Ikiwa wafu hawafufuki kabisa, kwa sababu gani watu wanabatizwa kwa ajili yao?

30Na sisi wenyewe, kwa nini tunahatarisha maisha yetu kila saa?

31Wandugu zangu, kila siku ninapatwa na hatari ya kufa. Na hii ni hakika sawa vile ninavyojivuna kwa ajili yenu katika kuungana kwangu na Yesu Kristo Bwana wetu.

32Ikiwa ni kwa nia ya kimutu, nimepigana na nyama wakali wa pori katika Efeso, jambo lile limenifalia nini? Kama wafu hawafufuki, basi: “Tukule na tukunywe, kwa maana kesho tutakufa.”

33Musidanganyike: “Warafiki wabaya wanaharibu tabia nzuri za watu.”

34Mugeuze mafikiri, murudie katika usawa, muache kufanya zambi. Ninasema neno hili kwa kuwapatisha haya, kwa sababu wamoja kati yenu hawamujui Mungu.

Mwili wa ufufuko

35Lakini labda kuko mutu anayeweza kuuliza: “Namna gani wafu watafufuka? Nao watakuwa na mwili wa namna gani wakati ule watakaporudia?”

36Wewe mujinga! Wakati unapopanda mbegu, mbegu ile haiwezi kuota isipokufa kwanza.

37Kile unachopanda si mumea muzima utakaopaswa kutokea nyuma, lakini ni punje tu, labda ya ngano au mbegu ingine fulani.

38Mungu anatokeza ndani ya ile punje umbo la mumea anaotaka; yeye anatokeza ndani ya kila mbegu umbo la kipekee.

39Miili ya viumbe vyote si sawa: watu wako na mwili wao wa kipekee, na nyama vilevile, na mwili wa ndege na samaki ni mbalimbali.

40Vilevile kuna miili ya mbinguni na miili ya dunia; nao uzuri wa miili ya mbinguni ni mbalimbali na uzuri wa miili ya dunia.

41Uzuri wa jua ni mbalimbali na uzuri wa mwezi, nao uzuri wa nyota ni mbalimbali, kwa maana hata nyota zinapishana uzuri vilevile.

42Itakuwa hivi vilevile wakati wafu watakapofufuka. Mwili unazikwa katika udongo katika hali ya kuharibika, lakini unapofufuka, unafufuka na hali ya kutoweza kuharibika

43na hali ya utukufu; nao unazikwa katika uzaifu, lakini unafufuka na nguvu.

44Wakati unapozikwa ni mwili wa kimutu, lakini unapofufuka unageuka mwili wa kiroho. Kama kuna mwili wa kimutu, basi kuna mwili wa kiroho vilevile.

45Kwa maana, Maandiko Matakatifu yanasema: “Mutu wa kwanza, Adamu, alikuwa kiumbe chenye uzima”; lakini Adamu wa mwisho ni Roho anayewapatia watu uzima.

46Si mwili wa kiroho unaotangulia lakini ni mwili wa kimutu, kisha ule wa kiroho unafuata.

47Adamu wa kwanza aliumbwa kwa udongo, yeye ni wa dunia, lakini Adamu wa pili alitoka mbinguni.

48Watu wa dunia wanafanana na yule aliyeumbwa kwa udongo, na watu wa mbinguni wanafanana na yule aliyetoka mbinguni.

49Na kama vile tulivyofanana na yule mutu aliyeumbwa kwa udongo, vilevile tutafanana na yule aliyetoka mbinguni.

50Wandugu zangu, muangalie, jambo ninalotaka kusema ni hili: kile kilichoumbwa kwa nyama na damu hakiwezi kupata urizi katika Ufalme wa Mungu katika hali ile, wala hakuna chenye hali ya kuharibika kinachoweza kuwa na hali ya kutoharibika.

51Sasa nitawaambia ninyi siri: sisi wote hatutakufa, lakini sisi wote tutabadilishwa

52kwa rafla, kama vile mutu anavyofunga jicho na kulifungua, wakati ngunga ya mwisho itakapolia. Kwa maana wakati itakapolia, wafu watafufuka na kupata kuwa katika hali ya kutoweza kufa tena, na sisi wote tutabadilishwa.

53Kwa maana sherti mwili huu wa kuharibika uvae mwili wa kutoharibika, na mwili wa kufa sherti uvae mwili wa kutokufa.

54Na wakati mwili huu wa kuharibika utakapovaa ule wa kutoharibika, nao mwili wa kufa utakapovaa ule wa kutokufa, halafu Maandiko Matakatifu haya yatatimia: “Kifo kimekomeshwa; kimeshindwa kabisa.”

55“Ewe kifo, ushindi wako uko wapi?

Ewe kifo, uwezo wako wa kuua uko wapi?”

56Kifo kinapata uwezo wa kuua kutokana na zambi, na zambi inapata uwezo wake kutokana na Sheria.

57Lakini tumushukuru Mungu anayetupatia ushindi kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo.

58Basi wandugu zangu wapenzi, musimame imara bila kutikisika. Muendelee kumutumikia Bwana siku zote, mukijua kwamba masumbuko munayopata kwa ajili ya Bwana hayatapita bure.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help