1Hili ni simulizi la Nehemia mwana wa Hakalia.
Mapaswa ya Nehemia juu ya YerusalemaIlitukia kwamba, nilipokuwa katika muji mukubwa wa Susani, katika mwezi wa Kisileu wa mwaka wa makumi mbili,
2Hanani, mumoja wa wandugu zangu, akakuja pamoja na sehemu ya watu toka katika inchi ya Yuda. Nikawauliza juu ya Wayuda wenzetu walioponyoka, ni kusema ambao hawakuhamishiwa Babeli na juu ya Yerusalema.
3Wao wakaniambia: “Wayuda walioponyoka na kubaki katika jimbo lile, wako katika taabu nao wanazarauliwa. Ukuta wa Yerusalema umebomolewa na milango yake imeteketezwa.”
4Niliposikia hayo nikaikaa chini na kulia, nikaomboleza kwa siku za kutosha. Nikafunga kula na kumwomba Mungu wa mbinguni,
5nikisema: “Ee Yawe, Mungu wa mbinguni, wewe ni Mungu unayekuwa mukubwa na wa kutisha, unashika agano lako na kutenda mema kwa wale wanaokupenda na kushika amri zako.
6Usikilize kwa uangalifu maombi yangu, na uniangalie mimi mutumishi wako, ninapokuomba kwa ajili ya watumishi wako, watu wa Israeli, usiku na muchana. Ninaungama zambi za watu wa Israeli, tulizofanya mbele yako. Mimi pamoja na watu wa jamaa yangu tumefanya zambi.
7Tumetenda mabaya mbele yako, hatujashika amri zako, masharti na maagizo yako uliyomwagiza mutumishi wako Musa.
8Kumbuka sasa lile ulilomwambia mutumishi wako Musa, uliposema: ‘Kama hamutakuwa waaminifu, nitawatawanya kati ya mataifa. Ang. Law 26.23
9Lakini mukinirudilia, mukishika amri zangu na kuzifuata hata ingawa nitakuwa nimewatawanya mbali kabisa, nitawarudisha pahali nilipochagua kuwa pahali pangu pa kuabudiwa.’ Ang. Kumb 30.1-5
10Watu wa Israeli ni watumishi wako na watu wako uliwakomboa kwa uwezo wako na mukono wako wenye nguvu.
11Ee Bwana, usikilize maombi yangu mimi mutumishi wako na ya watumishi wako wanaofurahia kukutii wewe. Ninakuomba unifanikishe leo, mimi mutumishi wako, na kunijalia kuhurumiwa na mufalme.”
Mimi nilikuwa na madaraka ya kumupa mufalme kinywaji.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.