Isaya 41 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Mungu anaahidi kuisaidia Israeli

1Mungu anasema hivi:

Enyi wakaaji wa mbali munyamaze munisikilize!

Enyi mataifa mujitie moyo;

mujitokeze na mujisemee,

na mukuje tuende pamoja kwa hukumu.

2Ni nani aliyemwita shujaa toka mashariki,

mutu ambaye anapata ushindi popote anapoenda?

Mimi ninayaweka mataifa katika mikono yake,

naye anawaponda wafalme chini ya miguu yake!

Upanga wake unawafanya kuwa kama mavumbi,

kwa upinde wake anawapeperusha kama maganda.

3Yeye anawakimbiza na kupita kwa usalama;

anaenda mbio bila kukanyaga chini.

4Nani aliyefanya yote haya yatendeke?

Ni nani aliyepanga wakati wa kila tukio?

Mimi Yawe nipo tangu mwanzo,

mimi nitakuwa hata milele.

5Wakaaji wa mbali wameona mambo niliyotenda, wakaogopa;

dunia yote inatetemeka kwa woga.

Watu wote wamekusanyika, wakakuja.

6Kila mumoja anamusaidia mwenzake akisema:

Ujipe moyo!

7Fundi anamusaidia mufuaji wa zahabu.

Naye anayelainisha sanamu kwa hama,

anamusaidia anayeiunga kwa misumari.

Wote wanasema: Ni vizuri sana!

Kisha wanaifunga kwa misumari isitikisike.

8Sikiliza ewe Israeli, mutumishi wangu,

wewe, Yakobo ambaye nimekuchagua,

wewe wa uzao wa Abrahamu, rafiki yangu;

9wewe niliyekuleta toka miisho ya dunia,

niliyekuita toka mbali kwa mipaka ya dunia,

wewe niliyekuambia: Wewe ni mutumishi wangu;

mimi sikukutupilia, lakini nilikuchagua.

10Basi, usiogope, mimi nipo pamoja nawe.

Usifazaike, mimi ni Mungu wako.

Nitakuimarisha na kukusaidia;

nitakulinda kwa mukono wangu wa ushindi.

11Kweli! Wote waliokukasirikia,

watapata haya na kufezeheka.

Wote wanaopingana nawe,

watakuwa wa bure na kuangamia.

12Utawatafuta hao wanaopingana nawe,

hautawaona tena;

wale wanaofanya vita nawe,

watakuwa wameangamia.

13Mimi ndiye Yawe, Mungu wako,

ndiye ninayeshika mukono wako.

Mimi ndiye ninayekuambia:

Usiogope, nitakusaidia.

14Enyi watu wa Yakobo zaifu kama mududu,

enyi Waisraeli, musiogope!

Nitawasaidia.

–Ni ujumbe wa Yawe.–

Mukombozi wenu ni yule Mutakatifu wa Israeli.

15Nitawafanya mukuwe kama chombo cha kupepeta,

chenye meno mapya na makali.

Mutaipepeta milima na kuipondaponda;

mutavisagasaga vilima kama maganda.

16Mutaipepeta milima hiyo,

nao upepo utaipeperushia mbali,

zoruba itaitawanya huko na huko.

Nanyi mutafurahi kwa sababu yangu Yawe;

mutaona utukufu kwa sababu yangu

Mungu Mutakatifu wa Israeli.

17Wamasikini na wakosefu wakitafuta maji lakini hawayapati,

wakiwa wamekauka koo kwa kiu,

mimi Yawe nitawajibu;

mimi Mungu wa Israeli, sitawaacha.

18Nitabubujisha mito kwenye milima mitupu,

na chemichemi katika mabonde.

Nitaigeuza jangwa kuwa ziwa la maji,

na inchi kuwa chemichemi za maji.

19Nitapanda miti kule katika jangwa:

mierezi, mivinje, mijohoro, na mizeituni;

nitaweka kule katika jangwa:

miberoshi, shindano na misunobari.

20Watu wataona jambo hilo,

nao watatambua na kuelewa kwamba

mimi Yawe nimetenda hayo,

mimi Mutakatifu wa Israeli nimefanya jambo hilo.

21Yawe, Mufalme wa Yakobo, anasema:

Enyi miungu ya mataifa, mulete maneno yenu,

mukuje mujitetee!

22Mujongee, mutuambie yatakayotukia.

Mutuambie matukio ya kwanza yalikuwa gani,

nasi tutafikiri juu yake.

Au mututangazie jinsi yatakavyotimia,

kusudi tujue yatakayokuja.

23Mutuambie yatakayotokea nyuma,

nasi tujue basi kama ninyi ni miungu.

Mufanye kitu chochote, chema au kibaya,

kusudi tushangae na kuogopa.

24Hakika, ninyi si kitu kabisa.

Hamuwezi kufanya kitu chochote.

Anayechagua kuwaabudu ninyi ni chukizo.

25Nimetokeza mutu toka kaskazini,

naye amekuja;

nimemuchagua mutu toka mashariki,

naye atalitaja jina langu.

Yeye atawakanyaga wafalme kama matope,

kama vile mufinyanzi anavyoponda udongo wake.

26Nani aliyetangaza haya tangu mwanzo,

hata sisi tupate kuyatambua?

Nani aliyetangulia kuyatangaza,

kusudi sasa tuseme, alisema ukweli?

Hakuna hata mumoja kati yenu aliyeyataja,

wala hakuna aliyesikia maneno yenu.

27Mimi ni yule wa kwanza. Nilitangaza kwa Sayuni,

nikapeleka Yerusalema mujumbe wa habari njema.

28Nimeangalia vizuri sana,

lakini simwoni mutu yeyote;

hakuna yeyote kati ya hao miungu anayeweza kushauri;

nikiuliza, hakuna anayeweza kunijibu.

29Miungu hiyo yote ni udanganyifu,

haiwezi kufanya kitu chochote;

sanamu zao ni upepo tu, hazina maana.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help