1Katika mwaka wa kumi na ine wa utawala wa mufalme Hezekia, mufalme Saniharibu wa Asuria aliishambulia miji yote yenye kuta ya inchi ya Yuda na kuinyanganya.
2Kisha mufalme wa Asuria alimutuma jemadari kutoka Lakisi na kundi kubwa kumwendea mufalme Hezekia. Jemadari yule alisimama karibu na mufereji wa birika linalokuwa upande wa juu katika barabara kubwa inayoelekea shamba la wafuaji wa nguo.
3Nao walikutana na Eliakimu mwana wa Hilkia, aliyekuwa musimamizi wa nyumba ya kifalme, Sebuna, aliyekuwa katibu, pamoja na mwandishi Yoa mwana wa Asafu.
4Halafu yule jemadari wa Asuria aliwaambia: “Mumwambie Hezekia kwamba mufalme mukubwa wa Asuria anamwuliza: Unategemea nini kwa kukazana kwako?
5Unazani kwamba maneno matupu ndiyo maarifa na nguvu katika vita? Ni nani unayemutegemea hata ukaniasi?
6Angalia sasa. Unategemea Misri, utete uliovunjika ambao utamuchoma mukono yeyote atakayeuegemea. Hivi ndivyo mufalme wa Misri anavyokuwa kwa wote wale wanaomutegemea. Ang. Eze 29.6-7
7Lakini hata kama mukiniambia ‘Tunamutegemea Yawe, Mungu wetu’, si huyohuyo ambaye Hezekia aliziharibu nafasi zake zote za kuabudu kwenye vilima pamoja na mazabahu zake na kuwaambia watu wa Yuda na Yerusalema: Munapaswa kuabudu mbele ya mazabahu hii ya Yerusalema tu?
8Basi, mufanye mapatano na bwana wangu mufalme wa Asuria. Mimi nitawapatia farasi elfu mbili, kama mutaweza kupata waaskari wapanda-farasi.
9Hata kama munategemea Misri kupata magari ya vita na waaskari wapanda-farasi, hamuwezi kumurudisha nyuma mutu mumoja wa cheo cha chini sana kati ya watumishi wa bwana wangu.
10Zaidi ya hayo, munafikiri nimekuja bila amri ya Yawe kwa kuishambulia na kuiangamiza inchi hii? Yawe ndiye aliyeniambia: ‘Ushambulie inchi hii na kuiangamiza!’ ”
11Kisha Eliakimu, Sebuna na Yoa wakamujibu yule jemadari: “Tafazali useme nasi kwa luga ya Kiaramea maana tunaielewa. Usiseme nasi kwa luga ya Kiebrania. Watu wanaokuwa juu ya ukuta wanasikia.”
12Yule jemadari akawaambia: “Munazani kwamba bwana wangu amenituma kutoa ujumbe huu kwa bwana wenu na kwenu tu? Maneno yangu ni vilevile kwa watu wanaoikaa juu ya ukuta! Bado kidogo wao kama vile ninyi watakula mavi yao wenyewe na kunywa mikojo yao wenyewe!”
13Kisha huyo jemadari akasimama, akalalamika na kusema kwa luga ya Kiebrania: “Musikilize maneno ya mufalme mukubwa, mufalme wa Asuria!
14Hivi ndivyo mufalme anavyosema: Musikubali Hezekia awadanganye, kwa sababu hataweza kuwaokoa.
15Musikubali awashawishi kusudi mumutegemee Yawe, akisema: ‘Yawe atatuokoa na muji huu hautatiwa katika mikono wa mufalme wa Asuria.’
16Musimusikilize Hezekia, maana mufalme wa Asuria anasema: Mukuwe na amani nami na kujitoa kwangu. Kisha kila mumoja wenu ataweza kula matunda ya mizabibu yake mwenyewe na matunda ya tini yake mwenyewe na kunywa maji ya kisima chake mwenyewe,
17mpaka nitakapokuja na kuwapeleka katika inchi kama hii yenu, inchi yenye ngano na divai, inchi yenye mukate na mashamba ya mizabibu.
18Musimusikilize Hezekia anapowadanganya akisema: ‘Yawe atatuokoa.’ Kuna yoyote kati ya miungu ya mataifa aliyeokoa inchi yake toka katika mikono ya mufalme wa Asuria?
19Iko wapi ile miungu ya Hamati na Arpadi? Iko wapi ile miungu ya Sefarwaimu? Imeokoa Samaria toka katika mikono yangu?
20Ni nani kati ya miungu ya inchi hizi aliyeokoa inchi zao toka katika mikono yangu. Yawe ataweza kuuokoa Yerusalema?”
21Lakini watu walinyamaza, wala hawakumujibu neno kama vile walivyoamuriwa na mufalme akisema: “Musimujibu.”
22Kisha Eliakimu mwana wa Hilkia aliyekuwa musimamizi wa nyumba ya kifalme, Sebuna aliyekuwa katibu, na Yoa mwana wa Asafu mwandishi, wakamwendea Hezekia na nguo zenye kupasuliwa, wakamwelezea maneno ya yule jemadari.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.