Ezekieli 48 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Eneo la makabila huko kaskazini

1Haya ndiyo majina ya makabila na sehemu zao: Kuanzia kwenye mupaka wa kaskazini kwenye barabara ya Hetiloni mpaka kuingia Hamati hata Hazorenoni unaokuwa katika Damasiki na Hamati upande wa kaskazini na kuendelea kutoka mashariki mpaka magaribi. Eneo hilo litakuwa la kabila la Dani.

2Eneo linalofuatana na la Dani, kutoka mashariki mpaka magaribi litakuwa la Aseri.

3Kabila la Nafutali, litapata eneo linalopakana na lile la Aseri, kutoka mashariki mpaka magaribi.

4Kisha eneo la kabila la Nafutali litafuata eneo la kabila la Manase, kutoka mashariki mpaka magaribi.

5Eneo linalopakana na eneo la Manase kutoka upande wa mashariki mpaka magaribi litakuwa la kabila la Efuraimu.

6Eneo linalopakana na eneo la Efuraimu kutoka mashariki mpaka magaribi litakuwa la kabila la Rubeni.

7Eneo linalopakana na eneo la Rubeni kutoka mashariki mpaka magaribi litakuwa la kabila la Yuda.

Eneo takatifu katikati ya inchi

8Kisha eneo la kabila la Yuda, utatenga eneo lenye urefu wa kilometre kumi na mbili na upana kama huohuo, kutoka kaskazini mpaka kusini, na urefu huohuo kutoka mashariki mpaka magaribi, sawasawa na eneo la kabila lolote. Hapo katikati ya eneo hilo patakuwa hekalu la Mungu.

9Eneo utakalotenga kwa ajili ya Yawe litakuwa lenye urefu wa kilometre kumi na mbili na nusu kwa kilometre kumi.

10Makuhani watakuwa na eneo lao katika eneo hilo. Eneo hilo litakuwa na urefu wa kilometre kumi na mbili na nusu kutoka mashariki mpaka magaribi, na kilometre tano kutoka kaskazini mpaka kusini. Hekalu la Mungu litakuwa katikati ya eneo hilo.

11Eneo hilo litakuwa kwa ajili ya makuhani wa uzao wa Zadoki, ambao walinitumikia kwa uaminifu na hawakuasi wakati Waisraeli walipoasi kama Walawi walivyofanya.

12Hilo litakuwa eneo lao takatifu kutoka katika eneo takatifu la inchi, eneo takatifu kabisa, litakalopakana na eneo la Walawi.

13Nao Walawi, eneo lao litakuwa upande wa kusini wa eneo la makuhani. Eneo hilo litakuwa na urefu wa kilometre kumi na mbili na nusu kutoka mashariki mpaka magaribi, na upana kilometre tano kutokea kaskazini mpaka kusini.

14Hakuna sehemu yoyote ya eneo hilo itakayouzishwa au kutolewa kwa mutu yeyote, kwa sababu eneo hilo ni takatifu kwa Yawe; nalo ni bora kuliko yote katika inchi.

15Ile sehemu ya eneo takatifu iliyobaki, yenye urefu wa kilometre kumi na mbili na nusu na upana kilometre mbili na nusu, hilo ni kwa matumizi ya kawaida ya muji: pahali pa kuishi na eneo la mashamba. Katikati yake kutakuwa muji,

16nao utakuwa wa muraba, kila upande metre elfu mbili mia mbili na makumi tano.

17Kuuzunguka muji, kutakuwa na eneo wazi lenye upana wa metre mia moja na makumi mbili na tano.

18Eneo ambalo litabaki kisha kujengwa kwa hekalu, upande wa kusini wa muji, kilometre tano kwa kilometre mbili na nusu upande wa mashariki, na kilometre tano kwa kilometre mbili na nusu upande wa magaribi, litakuwa eneo la walimaji kwa wakaaji wa muji.

19Watumishi wote katika muji wa kabila lolote la Waisraeli wanaweza kulima katika eneo hilo.

20Hivyo, eneo lote utakalotenga, ni kusema eneo takatifu pamoja na eneo la muji litakuwa la muraba, kilometre kumi na mbili na nusu kila upande.

21Eneo linalobaki katika pande zote za eneo takatifu na eneo la muji, ni kusema lile eneo lenye eneo muraba likiwa na kilometre kumi na mbili na nusu kwa kila upande tokea mashariki mpaka magaribi, kuelekea maeneo ya makabila, litakuwa la mufalme. Lile eneo takatifu ambamo hekalu la Mungu litakuwa katikati yake,

22na eneo la Walawi pamoja na lile eneo la muji, yatakuwa katikati ya eneo la mufalme. Eneo la mufalme litakuwa katika mupaka wa eneo la kabila la Yuda na eneo la kabila la Benjamina.

Urizi wa makabila mengine

23Makabila yaliyobaki yatagawanyiwa maeneo yao hivi: Kabila la Benjamina litapewa eneo kutoka mashariki mpaka magaribi.

24Eneo linalopakana na eneo la Benjamina kutoka upande wa mashariki kuelekea upande wa magaribi litakuwa la kabila la Simeoni.

25Eneo linalopakana na kabila la Simeoni kutoka upande wa mashariki kuelekea upande wa magaribi litakuwa eneo la kabila la Isakari.

26Eneo linalopakana na kabila la Isakari kutoka upande wa mashariki kuelekea upande wa magaribi, litakuwa eneo la kabila la Zebuluni.

27Eneo linalopakana na kabila la Zebuluni, kutoka mashariki kuelekea magaribi, litakuwa eneo la kabila la Gadi.

28Eneo linalopakana na kabila la Gadi kuelekea kusini, mupaka utatoka muji wa Tamari mpaka kwenye chemichemi za Meriba-Kadesi na kupitia upande wa mashariki ya Misri mpaka kwenye bahari ya Mediteranea.

29Hilo ndilo eneo la makabila ya Waisraeli. Humo ndimo watapewa maeneo yao, kila kabila eneo lake.

–Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.

Milango ya Yerusalema

30Muji Yerusalema utakuwa na ukuta ambao utakuwa na milango hii ya kutokea na kuingilia: Upande wa kaskazini urefu wa ukuta utakuwa metre elfu mbili mia mbili na makumi tano. Upande huo wa kaskazini Ang. Ufu 21.12-13

31utakuwa na milango mitatu: mulango wa Rubeni, mulango wa Yuda na mulango wa Lawi.

32Ukuta wa upande wa mashariki utakuwa na urefu wa metre elfu mbili mia mbili makumi tano. Upande huo utakuwa na milango mitatu: mulango wa Yosefu, mulango wa Benjamina na mulango wa Dani.

33Ukuta wa upande wa kusini utakuwa na urefu wa metre elfu mbili mia mbili na makumi tano. Upande huo utakuwa na milango mitatu: mulango wa Simeoni, mulango wa Isakari na mulango wa Zebuluni.

34Ukuta wa upande wa magaribi utakuwa na urefu wa metre elfu mbili mia mbili makumi tano. Upande huo nao utakuwa na milango mitatu: mulango wa Gadi, mulango wa Aseri na mulango wa Nafutali.

35Jumla ya urefu wa kuta zote ine utakuwa ni metre elfu kenda. Jina la muji kutokea sasa na kuendelea litakuwa: Yawe Yupo Hapa.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help