1Yesu akaingia katika chombo akavuka tena ziwa kwenda upande wa magaribi, naye akafika katika muji wake.
2Na kule wakamuletea mutu mwenye ugonjwa wa kupooza, akilala juu ya kipoyi. Yesu alipoona namna watu wale walivyomwaminia, akamwambia yule mwenye kupooza: “Mutoto wangu, ujipe moyo! Zambi zako zimesamehewa!”
3Halafu walimu wamoja wa Sheria waliokuwa pale wakajisemesha: “Mutu huyu anamutukana Mungu!”
4Naye Yesu akijua mafikiri yao, akawauliza: “Sababu gani munawaza maneno hayo mabaya?
5Kitu gani kinachokuwa chepesi kusema: ‘Zambi zako zimesamehewa’, au kusema: ‘Simama, utembee’?
6Basi, ninataka mujue kwamba Mwana wa Mutu yuko na mamlaka ya kusamehe zambi hapa katika dunia.” Kwa hiyo akamwambia yule mutu mwenye kupooza: “Simama, utwae kipoyi chako na uende kwako.”
7Na mutu yule akasimama na kwenda kwake.
8Watu walipoona jambo hilo wakaogopa na kumusifu Mungu aliyewapa watu mamlaka ya namna ile.
9Yesu alipokuwa akipita, akamwona mutu anayeitwa Matayo, akiikaa katika nyumba ya kulipishia kodi. Yesu akamwambia: “Unifuate!” Naye akasimama na kumufuata.
Yesu anamwita Matayo(Mk 2.13-17; Lk 5.27-32)10Nyuma Yesu akaikaa kula chakula ndani ya nyumba ya Matayo. Walipishaji wengi wa kodi na watenda mabaya wengine walikuwa wamekuja pale, nao waliikaa kula pamoja na Yesu na wanafunzi wake.
11Nao Wafarisayo walipoona mambo hayo, wakawaambia wanafunzi wake: “Kwa sababu gani mwalimu wenu anakula pamoja na walipishaji wa kodi na watenda mabaya?”
12Lakini Yesu alisikia vile walivyosema, na kwa hiyo akawaambia: “Wenye afya nzuri hawahitaji muganga lakini wale wanaokuwa wagonjwa.
13Muende kujifunza maana ya Maandiko Matakatifu yanayosema: ‘Ninataka huruma, lakini si sadaka zenu.’ Kwa maana sikukuja kuwaita wenye haki kunifuata, lakini watenda mabaya.”
14Wanafunzi wa Yoane Mubatizaji wakamufikia Yesu na kumwuliza: “Sababu gani sisi na Wafarisayo tunafunga kula chakula, lakini wanafunzi wako hawafungi?”
Ulizo juu ya kufunga kula chakula(Mk 2.18-22; Lk 5.33-39)15Yesu akawajibu: “Munafikiri kwamba warafiki za bwana-arusi wanaweza kufanya kilio wakati bwana-arusi angali pamoja nao? Hapana! Lakini kutakuwa siku bwana-arusi atakapoondoshwa kati yao; ni siku zile watafunga kula.
16“Hakuna mutu anayeshonea kiraka kipya juu ya nguo ya zamani. Kama anafanya vile, kile kiraka kipya kinapasua nguo ya zamani, na kupasuka kwake kunaongezeka zaidi.
17Vilevile hawatii divai mupya ndani ya machupa ya ngozi yenye kuzeeka. Wakifanya vile yale machupa yanapasuka, halafu divai inamwangika, nayo machupa yanapotea bure. Lakini inafaa kutia divai mupya ndani ya machupa mapya ya ngozi, navyo vyote vinalindwa vizuri.”
Binti ya mukubwa na mwanamuke aliyegusa nguo za Yesu(Mk 5.21-43; Lk 8.40-56)18Yesu alipokuwa hajamaliza kusema maneno hayo, mukubwa mumoja akafika, akapiga magoti mbele yake na kumwambia: “Binti yangu anakufa sasa hivi; lakini kuja, uweke mikono yako juu yake kusudi apate kufufuka.”
19Halafu Yesu akaondoka, akamufuata pamoja na wanafunzi wake.
20Na kulikuwa mwanamuke mumoja mwenye ugonjwa wa kutokwa na damu kwa muda wa miaka kumi na miwili. Yeye akakuja nyuma ya Yesu na kugusa upindo wa nguo yake,
21kwa maana alikuwa akijisemesha: “Kama nikigusa tu nguo yake, nitapona.”
22Naye Yesu alipogeuka, akamwona na kumwambia: “Binti yangu, ujipe moyo! Imani yako imekuponyesha.” Na mwanamuke yule akapona saa ile ile.
23Yesu alipofika kwa nyumba ya yule mukubwa, akaona wapiga muziki wakiimba nyimbo za kilio nalo kundi la watu wakifanya kelele.
24Halafu akasema: “Mutoke hapa. Binti huyu mudogo hakukufa, lakini analala tu.” Nao wakaanza kumuchekelea.
25Na watu wale walipokwisha kufukuzwa, Yesu akaingia ndani ya chumba, akashika mukono wa yule binti, naye akasimama.
26Habari za jambo hili zikaenea katika inchi ile yote.
Yesu anaponyesha vipofu wawili27Yesu akaondoka toka pale, naye alipokuwa katika njia, vipofu wawili wakamufuata wakilalamika, wakisema: “Utuhurumie, Ee Mwana wa Daudi!”
28Na wakati Yesu alipoingia ndani ya nyumba, wale vipofu wakamufikia. Naye akawauliza: “Munaamini kwamba ninaweza kuwafanyia jambo hilo?”
Nao wakamujibu: “Ndiyo, Bwana.”
29Halafu Yesu akagusa macho yao, akisema: “Ifanyike kwenu sawa vile munavyoaminia.”
30Nayo macho yao yakapona. Na Yesu akawaagiza kwa nguvu, akisema: “Angalisho, musimujulishe hata mutu mumoja jambo hili.”
31Lakini wakaenda na kuanza kutangaza habari za Yesu katika inchi ile yote.
Yesu anaponyesha bubu32Watu hao wawili walipokwisha kwenda, wakamuletea Yesu mutu mumoja bubu aliyeshikwa na pepo.
33Wakati Yesu alipokwisha kumufukuza yule pepo, yule bubu akaanza kusema. Nao watu wote wakashangaa na kusema: “Hatujaona jambo kama hili katika inchi yote ya Israeli!”
34Lakini Wafarisayo wakasema: “Ni mukubwa wa pepo ndiye anayemupa uwezo wa kufukuza pepo.”
Yesu anahurumia watu35Yesu alizunguka katika miji na vijiji vyote, akiwafundisha watu katika nyumba zao za kuabudia, akiwahubiri Habari Njema ya Ufalme. Aliponyesha magonjwa yote na uzaifu wa kila namna.
36Yesu alipoona kundi la watu, aliwasikilia huruma, kwa maana walikuwa wamesumbuka na kuregea, kama kondoo wasiokuwa na muchungaji.
37Halafu akawaambia wanafunzi wake: “Mavuno ni mengi, lakini wavunaji ni wachache.
38Basi muombe Bwana mwenyeji wa mavuno awatume wavunaji wengine kwa kuvuna mavuno yake.”
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.