1Kwa hiyo mutuhesabu kama watumishi wa Kristo, wanaoshugulika na ujumbe wa siri wa Mungu.
2Yanayohitajika kwa mwenye madaraka kama hayo, ni kuwa mwaminifu.
3Kwa ngambo yangu, si neno hata kidogo kuhukumiwa nanyi au na tribinali ya watu. Na hata mimi mwenyewe sijihukumu.
4Kweli zamiri yangu hainihukumu juu ya neno lolote, lakini hii si kusema kwamba mimi ni mwenye haki. Bwana ndiye anayenihukumu.
5Kwa hiyo musihukumu mutu mbele ya wakati uliopangwa; mungojee mpaka Bwana atakaporudia. Yeye ndiye atakayeonyesha wazi katika mwangaza mambo yote yaliyofichwa katika giza na kufunua nia za siri za watu. Halafu kila mutu atapokea sifa anayostahili toka kwa Mungu.
6Wandugu zangu, nimesema maneno haya nikitwaa mufano wa Apolo na wangu mimi mwenyewe kusudi yakuwe fundisho kwenu. Nilitaka kwamba kufuatana na mufano huu mujifunze maana ya masemi haya: “Musipite pembeni ya maandiko.” Hata mutu mumoja kati yenu asijivunie mutu fulani na kuzarau mwingine.
7Ni nani aliyekuweka kuwa mukubwa kuliko wengine? Si Mungu ndiye aliyekupa vitu vyote unavyokuwa navyo? Ikiwa ni hivi, kwa sababu gani unajivuna kama vile haukuvipewa kama zawadi?
8Sasa mumekwisha kupata vyote munavyohitaji! Mumekwisha kuwa watajiri! Munakuwa wafalme ingawa sisi hatuko wafalme. Heri mungekuwa kweli watawala kusudi nasi vilevile tupate kutawala pamoja nanyi.
9Kwa maana inaonekana kuwa Mungu ametufanya sisi mitume kuwa watu wenye hali ya chini kabisa. Tunahesabiwa kama watu wanaohukumiwa kufa mbele ya watu. Tumewekwa kama kitu cha kushangaza, kinachoangaliwa na dunia nzima, nao wamalaika na watu vilevile.
10Sisi ni wapumbafu kwa ajili ya Kristo, lakini ninyi ni wenye hekima katika kuungana kwenu na Kristo. Sisi ni zaifu, lakini ninyi ni wenye nguvu. Tunazarauliwa, lakini ninyi munaheshimiwa!
11Hata sasa, tunateswa na njaa na kiu, tunakosa nguo, tunapigwa, tunatangatanga bila makao.
12Tunasumbuka sana tukifanya kazi kwa mikono yetu wenyewe. Wakati tunapotukanwa, tunabariki; wakati tunapoteswa, tunavumilia;
13wakati tunaposingiziwa, tunajibu kwa upole. Hata sasa tunahesabiwa kama takataka za dunia, na kila mutu anatuangalia kama uchafu.
14Siwaandikii maneno haya kwa kuwapatisha haya, lakini kwa kuwaonya kama watoto wangu wapendwa.
15Hivi kuelekea maisha yenu na Kristo, hata mukiwa na walezi maelfu muko tu na baba mumoja. Kwa maana kuelekea maisha yenu na Yesu Kristo ni mimi niliyewazaa kwa njia ya kuwatangazia Habari Njema.
16Basi ninawasihi, mufuate mufano wangu.
17Ni kwa sababu hii ninawatumia ninyi Timoteo. Yeye ni mwana wangu mupendwa na mwaminifu mbele ya Bwana. Atawakumbusha kanuni ninazofuata katika maisha yangu na Yesu Kristo, nami ninazofundisha fasi zote katika makanisa yote.
18Watu wamoja kati yenu wanajivuna wakifikiri kwamba sitakuja kuwaona.
19Lakini nitakuja kwenu upesi Bwana akitaka. Basi pale nitajua maneno ya wale wanaojivuna na kujionea uwezo wao vilevile!
20Kwa maana kazi ya Ufalme wa Mungu haionyeshwi kwa njia ya kusema tu, lakini vilevile kwa njia ya matendo ya uwezo.
21Basi munataka nini? Nifike kule kwenu, nikikuja na fimbo au na moyo unaojaa upendo na upole?
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.