1Kisha nikaona malaika mwingine mwenye nguvu aliyeshuka toka mbinguni; vazi lake lilikuwa wingu, kofia la kichwani pake lilikuwa upindi wa Mungu, uso wake ulikuwa kama jua, miguu yake ilikuwa kama nguzo zenye moto.Yohana anameza kitabu kidogo.
8Ndipo, ile sauti, niliyoisikia toka mbinguni, iliposema tena nami kwamba: Nenda, ukitwae kile kitabu kidogo kilichokuwa kimefunuka, kilichomo mkononi mwa malaika aliyesimama mguu mmoja baharini na mmoja nchini!Ufu. 10:2,4.
9Nikaenda kwa yule malaika, nikamwambia, anipe kile kitabu kidogo. Naye akaniambia: Kitwae, kile! Kitakutia uchungu tumboni mwako, lakini kinywani mwako kitakuwa kitamu kama asali.Ez. 3:1-4.
10Nikakitwaa kile kitabu kidogo mkononi mwa yule malaika, nikakimeza, nacho kilikuwa kitamu kama asali kinywani mwangu; lakini nilipokwisha kukimeza nikatiwa uchungu tumboni mwangu.
11Wakaniambia: Wewe imekupasa kufumbulia tena makabila mengi na wamizimu wengi na wenye misemo mingi na wafalme wengi.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.