Mashangilio 16 - Swahili Roehl Bible 1937

Mungu ni mali kuzipita zote.Fumbo la Dawidi.

1Unilinde, Mungu! Kwani nimekukimbilia.

2Nimemwambia Bwana: Wewe u bwana wangu; hakuna nionacho kuwa chema kisichotoka kwako.Sh. 73:25.

3Nao watakatifu waliopo katika nchi nimewaambia: Hawa ndio wakuu wa kweli, ndio wanipendezao kabisa.

4Maumivu yao wakimbiliao mwingine yatakuwa mengi; sitavimimina vinywaji vyao vya tambiko, maana ni vyenye damu, wala majina yao sitayatia tena midomoni mwangu.

5Bwana ni fungu langu, nililolitwaa, tena ni kinyweo, nilichopewa; wewe unanishikizia niliyopatiwa nilipopigiwa kura;Omb. 3:24.

6kamba zake ziliponiangukia niligawiwa pazuri, hilo fungu, nililolitwaa, linapendezeka kweli.

7Nitamkuza Bwana aniongozaye, mafigo yangu hunionya hivyo hata usiku.Sh. 4:5; 17:3.

8*Bwana na anisimamie kila, nitakapokuwa, awe kuumeni kwangu, nisitikisike.

9Kwa hiyo moyo wangu hufurahi, nayo yaliyo utukufu wangu hushangilia, hata mwili wangu utatulia kwa kuwa na kingojeo.1 Mose 49:6.

10Kwani hutaiacha roho yangu, ipotee kuzimuni, wala hutamtoa akuchaye, apate kuoza kaburini.Tume. 2:25-32; 13:35-37.

11Unanitambulisha njia iendayo penye uzima, utanishibisha furaha zilizopo usoni pako; mkono wako wa kuume hutoa kale na kale yapendezayo.*

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help