1Na atukuzwe Bwana aliye mwamba wangu! Ndiye aliyeifundisha mikono yangu kupiga vita, ijue hata kupiga konde kwenye mapigano.
3Bwana, mtu ndio nini, ukimjua? Mwana wa mtu naye, usipomsahau?
5Bwana, ziinamishe mbingu zako, utelemke! Iguse milima, itoke moshi!
9Mungu, nitakuimbia wimbo mpya pamoja na kukupigia pango lenye nyuzi kumi.
12Wana wetu wa kiume katika ujana wao tunawaombea, wakue kama miti ya kupandwa iliyotunzwa vizuri! Nao wana wetu wa kike na wawe kama nguzo zilizochorwa vizuri kuwa mapambo yao majumba matukufu.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.