1Boazi akapanda kwenda langoni pa mji, akakaa huko. Mara yule mwingiliaji, Boazi aliyemtaja, akapita; ndipo, alipomwambia: Njoo, wewe bwana fulani, ukae hapa! Akaacha kwenda, akaja kukaa.
2Kisha akachukua watu kumi walio wazee wa mjini, akawaambia: Kaeni hapa! Nao wakakaa.
3Akamwambia huyo mwingiliaji: Fungu la shamba lililokuwa lake ndugu yetu Elimeleki, Naomi aliyerudi kutoka kwenye mbuga za Moabu anataka kuliuza.
4Nami nimesema, niyaeleze masikioni pako kwamba: Linunue machoni pao wanaokaa hapa napo machoni pao wazee wa ukoo wangu! Kama unataka kulikomboa, haya! Likomboe! Kama hutaki kulikomboa, niambie, nijue! Kwani kuliko wewe hakuna awezaye kulikomboa, mimi mwenyewe ni nyuma yako. Akasema: Basi, mimi nitalikomboa.
13Ndivyo, Boazi alivyomchukua Ruti, akawa mkewe, akaingia nyumbani mwake, Bwana akampa kuwa mwenye mimba, akazaa mtoto wa kiume.(18-22: Mat. 1:3-6.)
18Hawa ndio walio wa uzao wa Peresi: Peresi alimzaa Hesironi,
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.