Mashangilio 50 - Swahili Roehl Bible 1937

Tambiko la kweli.(Taz. 1 Sam. 15:22.)Wimbo wa Asafu.

1Bwana Mungu aliye Mungu kweli alisema, akaziita nchi, akianzia maawioni kwa jua, afike nako machweoni kwake.

16Lakini asiyemcha Mungu humwambia: Sababu gani unayasimulia maagizo yangu? Nacho kinywa chako kinayasemaje maneno ya Agano langu?Rom. 2:21-23.

17Nawe unachukizwa unapoonywa, nayo maneno yangu unayatupia nyuma.

18Ukiona mwizi, ni rafiki yako, tena hufanya bia nao walio wazinzi.Ef. 5:11.

19Kinywa chako unakisemesha yaliyo mabaya, ulimi wako hutunga madanganyo.

20Ukikaa na ndugu yako unamsengenya, naye mtoto wa mama yako unamtukana.

21Hivyo ndivyo, ulivyovifanya, nikavinyamazia; ndipo, uliponiwazia kuwa sawa kama wewe. Kwa hiyo ninakuonya nikivitolea machoni pako.Sh. 73:11.

22Nanyi mliomsahau Mungu, yatambueni, nisije kuwararueni, pasiwepo mponya!

23Kunishukuru ndio ng'ombe ya tambiko initukuzayo; hiyo ni njia ya kumwonyesha mtu wokovu wa Mungu.*

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help