Mifano 14 - Swahili Roehl Bible 1937

Werevu wa kweli unatukuzwa.

1Werevu wa kweli wa wanawake huzijenga nyumba zao,

lakini ujinga wao huzibomoa kwa mikono yao wenyewe.

2Ashikaye njia inyokayo humcha Bwana,

lakini azipotoaye njia zake humbeza.

3Kinywani mwa mjinga imo fimbo ya majivuno,

lakini midomo ya werevu wa kweli huwalinda.

4Pasipo ng'ombe zizi hukaa likiwa safi,

lakini mapato huwa mengi, nguvu za ng'ombe zinapotumiwa.

5Shahidi mwenye kweli haongopi,

asemaye maneno ya uwongo ni shahidi mwenye uwongo.

6Mfyozaji akitafuta werevu wa kweli haupati,

lakini mtambuzi hupata upesi kujua maana.

7Toka kwa mtu aliye mjinga!

Kwani kwake huoni midomo ijuayo maana.

8Werevu wa kweli wa mtu aerevukaye humtambulisha njia yake,

lakini ujinga wa wapumbavu huwadanganya.

9Wajinga hufyoza wakikora manza,

lakini wanyokao hupendezana.

10Moyo wenyewe hujua uchungu wa roho yake,

hata katika furaha yake mwingine hajitii humo.

11Nyumba zao wasiomcha Mungu hubomolewa,

lakini mahema yao wanyokao yatachanua.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help