4 Mose 4 - Swahili Roehl Bible 1937

Kazi za Walawi.

1Bwana akamwambia Mose na Haroni kwamba:

2Fanyeni hesabu ya wana wa Kehati na kuwatoa kwao wana wa Lawi walio wa udugu wao wa milango ya baba zao.

3Wao wa miaka thelathini na zaidi mpaka miaka hamsini ndio wanaofaa wote kuuingia utumishi huo, wafanye kazi za humo Hemani mwa Mkutano.

21Bwana akamwambia Mose kwamba:

22Fanya hesabu ya wana wa Gersoni nao walio wa milango ya baba zao na wa udugu wao.

23Uwakague walio wenye miaka thelathini na zaidi mpaka miaka hamsini, ndio wanaofaa wote kuuingia utumishi, wafanye kazi za kutumikia Hemani mwa Mkutano.

24Hizi ndizo kazi zao walio wa udugu wa Gersoni za kutumika na za kuchukua mizigo:

25na wayachukue mazulia ya Kao, na Hema la Mkutano na chandalua chake na chandalua cha ngozi za pomboo kilichoko juu yake na pazia la hapo pa kuliingilia Hema la Mkutano,

26na nguo za uani na pazia la hapo pa kuingia langoni kwa ua, unaolizunguka Kao na meza ya kuteketezea ng'ombe ya tambiko, na kamba zao na vyombo vyote vya utumishi wao, nayo yote yapasayo kufanywa nao na wayafanye.

27Utumishi wote wa wana wa Gersoni, kama ni kuichukua mizigo iwapasayo yote, au kama ni kuzifanya kazi ziwapasazo zote, ufanyike kwa kuagizwa na Haroni na wanawe; ninyi mwaweke kwa kuzignlia kazi za mizigo yao yote.

28Hizi ndizo kazi za utumishi wao walio wa udugu wa wana wa Gersoni wa kutumikia Hemani mwa Mkutano, naye atakayewaangalia ni Itamari, mwana wa mtambikaji Haroni.

29Uwakague nao wana wa Merari walio wa udugu wao wa milango ya baba zao:

30uwakague walio wa miaka thelathini na zaidi mpaka miaka hamsini, ndio wanaofaa wote kuuingia utumishi, wafanye kazi za kutumikia Hemani mwa Mkutano.

31Hizi ndizo kazi zao za kuiangalia mizigo yao, nao huo ndio utumishi wao wote wa kufanya Hemani mwa Mkutano: kuzichukua mbao za Kao na misunguo yake na nguzo zake na miguu yake,

32na nguzo zinazouzunguka au na miguu yao na mambo zao na kamba zao na vyombo vyao vyote, wafanye yote yaupasayo utumishi wao. Navyo vyombo vya kuviangalia, wakivichukua, mwape na kuvitaja kila kimoja jina lake.

33Hizi ndizo kazi za utumishi wao walio wa udugu wa wana wa Merari, wazifanye za kutumikia Hemani mwa Mkutano, naye mkuu wao awe Itamari, mwana wa mtambikaji Haroni.

Hesabu ya Walawi.

34Kwa hiyo Mose na Haroni na wakuu wa mkutano wakawakagua wana wa Kehati walio wa udugu wao na wa milango ya baba zao;

35waliokuwa wenye miaka thelathini na zaidi mpaka miaka hamsini, ndio waliofaa wote kuuingia utumishi, wafanye kazi za kutumikia Hemani mwa Mkutano.

36Jumla yao walio wa udugu wao walikuwa watu 2750.

37Hii ndiyo jumla yao wote wa udugu wa Wakehati waliotumikia Hemani mwa Mkutano, Mose na Haroni waliowakagua kwa amri, Bwana aliyompa Mose.

38Wana wa Gersoni wakakaguliwa nao walio wa udugu wao na wa milango ya baba zao,

39waliokuwa wenye miaka thelathini na zaidi mpaka miaka hamsini, ndio waliofaa wote kuuingia utumishi, wafanye kazi za kutumikia Hemani mwa Mkutano.

40Jumla yao walio wa udugu wao na wa milango ya baba zao walikuwa watu 2630.

41Hii ndiyo jumla yao wote wa udugu wa wana wa Gersoni waliotumikia Hemani mwa Mkutano, Mose na Haroni waliowakagua kwa amri ya Bwana.

42Ndugu za wana wa Merari wakakagulia nao walio wa udugu wao na wa milango ya baba zao,

43waliokuwa wenye miaka thelathini na zaidi mpaka miaka hamsini, ndio waliofaa wote kuuingia utumishi, wafanye kazi za kutumikia Hemani mwa Mkutano.

44Jumla yao walio wa udugu wao walikuwa watu 3200.

45Hii ndiyo jumla yao walio wa udugu wa wana wa Merari, Mose na Haroni waliowakagua kwa amri, Bwana aliyompa Mose.

46Hawa ndio Walawi wote waliokaguliwa, Mose na Haroni na wakuu wa Waisiraeli waliowakagua, waliokuwa wa udugu wao na wa milango ya baba zao,

47ndio waliokuwa wenye miaka thelathini na zaidi mpaka miaka hamsini, nao ndio wote waliofaa kufanya kazi za kuutumikia huo utumishi nao utumishi wa kuchukua mizigo Hemani mwa Mkutano.

48Jumla yao walikuwa watu 8580.

49Kwa amri, Bwana aliyompa Mose, aliwakagua na kumweka kila mtu mmoja penye kazi yake ya utumishi na penye mzigo wake wa kuuchukua; nao wakawekwa vivyo hivyo, kama Bwana alivyomwagiza Mose.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help