Mashangilio 123 - Swahili Roehl Bible 1937

Kumtazamia Mungu.Wimbo wa kupapandia Patakatifu.

1Nimeyainua macho yangu na kuyaelekeza kwako, ukaaye mbinguni.

2Kama macho ya watumishi yanavyoitazama mikono ya bwana zao, au kama macho ya mjakazi yanavyoitazama mikono ya bibi yake, hivyo macho yetu humtazama Bwana Mungu wetu, hata atuhurumie.

3Tuhurumie, Bwana! Tuhurumie! Kwani tumeshiba sana mabezo.

4Roho zetu zimeshiba sana masimango yao wanaokula vya urembo, nayo mabezo yao wenye majivuno.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help