1Hawa ndio watambikaji na Walawi waliorudi milimani kwao pamoja na Zerubabeli, mwana wa Saltieli, na Yesua: Seraya, Yeremia, Ezera,Boma la Yerusalemu linaeuliwa.
27Walipotaka kulieua boma la Yerusalemu wakawatafuta Walawi mahali pao po pote, wawapeleke Yerusalemu kufanya mweuo na furaha kwa kushukuru na kuimbia matoazi na mapango na mazeze.
28Wakakusanyika wana wao walio waimbaji wakitoka katika nchi iliyouzunguka Yerusalemu na viwanjani kwa Netofa
29na Beti-Gilgali na mashambani kwenye Geba na Azimaweti; kwani kwenye vile viwanja ndiko, waimbaji walikojijengea kuzunguka Yerusalemu.
30Watambikaji na Walawi walipokwisha kujitakasa, wakawatakasa watu na malango na boma.
31Kisha nikawapeleka wakuu wa Yuda bomani juu, nikasimama hapo na makundi mawili makubwa ya kushukuru, moja likaenda ukutani juu kufika penye lango la Jaani.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.