1*Sasa sikia mtumishi wangu Yakobo!
Nawe Isiraeli, niliyemchagua!
2Hivi ndivyo, anavyosema Bwana aliyekuumba,
aliyekutengeneza tumboni mwa mama, anayekusaidia:
Usiogope, mtumishi wangu Yakobo,
nawe Isiraeli uongokaye, niliyemchagua!
3Kwani nitamwaga maji panapo kiu, nitokeze mito pakavu,
nitaimwaga Roho yangu kwao walio uzao wako,
nayo mbaraka yangu kwao walio miche yako.
4Watakuwa kama majani kwenye maji
au kama mifuu kwenye mito yenye maji.
5Huyu atasema: Mimi ni wake Bwana,
naye mwenziwe atajiita kwa jina la Yakobo,
naye mwingine ataandika mikononi mwake: Wa Bwana,
mwingine atajivunia jina la Isiraeli,
Ujinga wa matambiko ya kimizimu.6Hivi ndivyo, anavyosema Bwana, mfalme wa Isiraeli,
aliye mkombozi wake, yeye Bwana Mwenye vikosi:
Mimi ni wa mwanzo na wa mwisho,
pasipo mimi hakuna Mungu.*
7Yuko nani anayefanana na mimi?
Na apaze sauti, ayatangaze!
Tena anieleze, kama ni kwa sababu gani,
nikiweka ukoo wa watu kuwa wa kale na kale.
Hata yajayo nayo yatakayokuja na wayatangazie watu!
8Msistuke, wala msitetemeke!
Kumbe sikukuambia hayo toka kale na kuyatangaza?
Ninyi m mashahidi wangu: Yuko Mungu pasipo mimi?
Hakuna mwamba mwingine, nisioujua.
9Watengenezao vinyago wote si kitu, navyo viumbe vyao vya kupendeza havifai, wanaovishuhudia wenyewe hawaoni, wala hawatambui kazi, ambazo vilizifanya, kusudi wapatwe na soni.
10Ni nani aliyetengeneza mungu na kuyeyusha kinyago kisichofaa kitu?
22Nimeyatowesha mapotovu yako kama wingu,
nayo makosa yako kama kungugu.
Rudi kwangu! Kwani nimekukomboa.
23Shangilieni, mbingu, ya kuwa Bwana ameyatimiza!
Pigeni kelele, vilindi vya kuzimuni!
Pigeni shangwe na kupaza sauti,
milima na misitu na miti yote iliyomo!
Kwani Bwana amemwokoa Yakobo,
nako kwake Isiraeli anautokeza utukufu wake.
24Hivi ndivyo, anavyosema Bwana, mkombozi wako,
aliyekutengeneza tumboni mwa mama:
Mimi Bwana niliyafanya yote.
Mimi nilipoziwamba mbingu peke yangu,
nikazitanda hata nchi,
yuko nani aliyekuwa kwangu?
25Ndege, wapuzi wanazoziona, nazibezesha,
nao waaguaji nawalevya,
nao walio werevu wa kweli nawarudisha nyuma,
ujuzi wao naugeuza kuwa ujinga.
26Neno la mtumishi wake hulisimamisha,
nayo mashauri ya wajumbe wake huyatimiza.
Ni yeye auambiaye Yerusalemu: Na ukaliwe!
Nayo miji ya Yuda anaiambia: Jengweni!
Nami nitayasimamisha mabomoko yao!
27Kilindi cha maji anakiambia: Kauka!
mimi nitaipwelesha mito yako.
28Yeye ndiye anayemwambia Kiro:
Huyu ndiye mchungaji wangu
atakayeyatimiza mapenzi yangu yote.
Hivyo Yerusalemu utajengwa,
nalo Jumba takatifu litawekewa misingi.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.