1Kwenye mito ya Babeli twalikaa na kulia tulipoikumbuka Sioni,
2katika mifuu iliyoko kule twaliyaangika mazeze yetu.
3Kwani kule waliotuteka walitushurutisha kuimba nyimbo, wao waliotuumiza walitaka, tuwachezee, wakasema: Tuimbieni wimbo wa Sioni!
4Lakini tungaliwezaje kuimba wimbo wa Bwana katika nchi ya ugeni?
5Kama ningekusahau, Yerusalemu, nao mkono wangu wa kuume na usahauliwe!
8Wewe binti Babeli, utakuwa mahame tu. Mwenye shangwe ndiye atakayekulipisha hayo matendo yako, uliyotutendea sisi.
9Mwenye shangwe ndiye atakayewakamata watoto wako wachanga na kuwaponda mwambani.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.