Mashangilio 125 - Swahili Roehl Bible 1937

Mungu huwalinda walio wake.Wimbo wa kupapandia Patakatifu.

1Wamwegemeao Bwana hufanana nao mlima wa Sioni, hautikisiki, unakaa kale na kale.

2Kama milima inavyouzunguka mji wa Yerusalemu, ndivyo, Bwana anavyowazunguka walio ukoo wake kuanzia sasa hata kale na kale.

3Kwani bakora yao wasiomcha Mungu haitashika uflame wa kulitawala fungu lao walio waongofu, kusudi waongofu wasiipeleke mikono yao kushika yenye mapotovu.

4Bwana, walio wema wafanyizie mema, nao wanyokao mioyo!

5Lakini wao wazigeuzao njia zao kuwa za kuptokapotoka Bwana an awaache, wajiendee pamoja nao wafanyao maovu! Utengemano na uwakalie wao Waisiraeli!

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help