1Kweli, ninyi tu ndio walio watu,
2werevu wa kweli utakufa nao, mtakapokufa ninyi.
3Mimi nami ninazo akili kama ninyi, sikupungukiwa na akili, ninyi mnishinde, yuko nani asiyeyajua mambo kama hayo?
4Mtu wa kuchekwa na wenziwe ni mimi, mimi niliyemwita Mungu, akaniitikia; kweli mwongofu asiyekosa kabisa ni mtu wa kuchekwa.
5Atesekaye hubezwa moyoni mwake naye akaaye na kutulia, yuko tayari kuwasukuma wajikwaao miguu.
6Mahema yao wapokonyi hutengemana, nao wamkasirishao Mungu hukaa na kutulia, ndio, Mungu anaowatia mengi mikononi mwao.
7Haya! Uliza nyama, wakufundishe, nao ndege wa angani, wakueleze!
8Au sema na nchi yenyewe, nayo itakufundisha! Hata samaki wa baharini watakusimulia mambo.
9Yuko nani asiyeyajua haya yote, ya kuwa mkono wa Mungu ndio ulioyatengeneza haya?
10Mkononi mwake zimo roho zao hao nyama wote, zimo nazo pumzi zao wote wenye miili ya kimtu.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.