Waamuzi 5 - Swahili Roehl Bible 1937

Shangilio la Debora na Baraka.

1Siku ile Debora na Baraka, mwana wa Abinoamu, wakaimba kwamba:

2Kwa kuwa walikuwako waliowaongoza Waisiraeli, kwa kuwa nao watu wamejitoa wenyewe, kwa hiyo mtukuzeni aliye Bwana!

3Sikieni, ninyi wafalme! Sikilizeni, ninyi watawalaji! Mimi, mimi mwenyewe na nimwimbie Bwana, na nimshangilie Bwana Mungu wa Isiraeli!

4Bwana, ulipotoka Seiri, ulipopita mashambani kwa Edomu, nchi ikatetemeka, mbingu nazo zikanyesha, mawingu nayo yakanyesha mvua.

6Siku za Samugari, mwana wa Anati, barabara zilikuwa zimekufa, hata siku za Yaeli; nao walioshika njia hupitia zile za kupotokapotoka.

9Moyo wangu huwaelekea waongozi wa Waisiraeli waliojitoa wenyewe miongoni mwa watu. Mtukuzeni aliye Bwana!

10Ninyi mpandao punda weupe, nanyi mkaliao mazulia, nanyi mtembeao njiani: yafikirini mioyoni!

Kisha nchi ikapata kutulia miaka 40.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help