3 Mose 1 - Swahili Roehl Bible 1937

Ng'ombe za tambiko za kuteketezwa nzima.

1Bwana akamwita Mose, akasema naye toka Hemani mwa Mkutano kwamba:

2Waambie wana wa Isiraeli na kuwaagiza hivyo: Mtu wa kwenu akitaka kumpelekea Bwana matoleo ya nyama wa kufuga sharti hayo matoleo yenu myatoe katika ng'ombe au katika mbuzi na kondoo.

3Kama toleo lake ni ng'ombe, anayemtoa kuwa ng'ombe ya tambiko ya kuteketezwa nzima, sharti atoe dume asiye na kilema, ampeleke pa kuliingilia Hema la Mkutano, Bwana apate kupendezwa naye.

10Kama toleo lake, analolitoa kuwa ng'ombe ya tambiko ya kuteketezwa nzima, ni nyama mdogo kama kondoo au mbuzi sharti apeleke dume asiye na kilema.

11Amchinje mbele ya Bwana kando ya meza ya kutambikia upande wake wa kaskazini, nayo damu yake wana wa Haroni walio watambikaji na wainyunyize pande zote juu ya meza ya kutambikia.

12Kisha amchangue, naye mtambikaji avipange vipande vyake pamoja na kichwa chake na mafuta yake juu ya moto uliowashwa mezani pa kutambikia.

13Lakini matumbo na miguu na aioshe kwa maji, kisha mtambikaji atayatoa yote kwa kuyachoma moto yote yaliyowekwa juu ya meza ya kutambikia. Ndivyo, naye nyama mdogo anavyokuwa ng'ombe ya tambiko ya kuteketezwa nzima, ndio moto wenye mnuko wa kumpendeza Bwana.

14Kama toleo lake, analomtolea Bwana kuwa ng'ombe ya tambiko ya kuteketezwa nzima, ni ndege, basi, sharti apeleke hua au kinda la njiwa manga.

15Naye mtambikaji atampeleka mezani pa kutambikia, atamvunja kichwa chake, apate kumchoma moto mezani pa kutambikia, lakini damu yake sharti idondoke ukutani pake meza ya kutambikia.

16Kisha akiondoe kibofu chake cha koo pamoja na machafu yaliyomo, akitupe majivuni kando ya meza ya kutambikia upande wa maawioni kwa jua.

17Kisha ampasue kidogo mabawani, lakini asiyatenge! Kisha mtambikaji amchome moto mezani pa kutambikia juu ya kuni zilizowekwa juu ya moto. Ndivyo, naye ndege anavyokuwa ng'ombe ya tambiko ya kuteketezwa nzima, ndio moto wenye mnuko wa kumpendeza Bwana.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help