Mashangilio 58 - Swahili Roehl Bible 1937

Kukemea waamuzi wasio wa kweli.Kwa mwimbishaji. Fumbo la Dawidi la kuimba kama wimbo wa kwamba: Usiangamize!

1Ni vya kweli hivyo, mnavyohukumu, ninyi wakuu? nayo maamuzi yenu yananyoka, ninyi wana wa watu?

6Mungu yavunje meno yao vinywani mwao! Nayo magego ya wana wa simba yang'oe, Bwana!

7Sharti wakauke kama maji yanayojiendea tu, mishale yao sharti iwe, kama haina chembe, watakapoielekeza!

8Wawe kama kovya linalokwenda na kuyeyuka, au kama mimba ya mwanamke iharibikayo pasipo kuona jua.

9Hivyo nayo miiba yenu ikiwa haijakomaa penye miti yao, ataipeperusha kwa ukali wa moto, ijapo iwe mibichi!

10Mwongofu atafurahi akiyaona malipizi hayo, ataiogesha miguu yake katika damu yake asiyemcha Mungu.

11Ndipo, watu watakaposema: kumbe mwongofu hupata! Kumbe yuko Mungu ahukumuye katika nchi!

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help