1Yuko mwerevu wa kweli atakayejibu yenye ujuzi ulio kama upepo?
2Au yuko atakayelijaza tumbo lake upepo utokao maawioni kwa jua?
3Atamwonya mwenziwe kwa maneno yasiyofaa? Au atajisemea tu kwa mapuzi yasiyompatia mtu kitu?
4Kisha wewe unatangua kicho kiwacho chote, nayo mawazo ya kumnyenyekea Mungu unayabeua.
5Manza, ulizozikora, zinakifunza kinywa chako, ukachagua ulimi usemao yenye ujanja.
6Kinachokuumbua kuwa mwovu, si mimi, ni kinywa chako, nayo midomo yako ndiyo inayokusuta.
7Je? Mtu wa kwanza aliyezaliwa ni wewe? Au ulitoka tumboni mwa mama, milima ilipokuwa haijawa?
8Je? Ulizisikiliza njama za Mungu? Je? Ndiko, ulikouvuta werevu wa kweli, ukujie wewe?Jibu la nne la Iyobu: Anamtolea Mungu ukiwa wake.
Iyobu akajibu akisema:
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.