1Sisi Paulo na Silwano na Timoteo tunawaandikia ninyi mlio wateule wa Tesalonike katika Mungu Baba na Bwana Yesu Kristo. Upole uwakalie na utengemano!Jinsi Watesalonike walivyoipokea mbiu njema.
2Tunamshukuru Mungu siku zote kwa ajili yenu nyote. Nasi hatuachi kuwakumbuka katika kuomba kwetu
3tukikumbuka mbele ya Mungu aliye Baba yetu, mnavyofanya kazi kwa kumtegemea, tena mnavyojisumbua, mpate kupendana, tena mnavyovumilia na kumngojea Bwana wetu Yesu Kristo.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.