1E Bwana, sikia jambo liongokalo! Yaitikie malalamiko yangu! Sikiliza nikuombayo na midomo isiyodanganya!
2Wewe uniamulie shauri langu, maana macho yako huyatazama yaliyonyoka.
3Umeujaribu moyo wangu na kunikagua usiku, ukaning'aza motoni pasipo kuona kibaya; nikajikaza moyoni kwa ajili ya kinywa changu, kisipite mpaka.
13Inuka, e Bwana! Umjie mbele, upate kumbwaga! Kwa upanga wako iokoe roho yangu mikononi mwake asiyekucha!
14Mkono wako, Bwana, uniokoe mikononi mwa waume, ambao kiume chao ni cha dunia hii, fungu lao nalo liko nchini tu. Matumbo yao uyajaze mali zako, washibe pamoja na wana wao, tena watakazozisaza waziachie hao watoto wao!Luk. 16:25; Fil. 3:19.
15Lakini mimi kwa hivyo, nilivyo mwongofu, nautazamia uso wako, niamkiapo nipate kushiba kwa kukuona, ulivyo wewe.
Tukuzo la wokovu.(2-51: 2 Sam. 22:2-51.)Kwa mwimbishaji. Wa Dawidi, mtumwa wa Bwana. Alimwambia Bwana maneno ya wimbo huu siku ile, Bwana alipomponya mikononi mwa adui zake wote namo mikononi mwa Sauli.Akasema
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.