Mateo 8 - Swahili Roehl Bible 1937

Mwenye ukoma.(1-4: Mar. 1:40-44; Luk. 5:12-14.)

1*Alipotelemka mlimani, makundi mengi ya watu wakamfuata.

2Mara akaja mwenye ukoma, akamwangukia akisema: Bwana, ukitaka waweza kunitakasa.

3Ndipo, Yesu aliponyosha mkono, akamgusa akisema: Nataka, utakaswe. Mara ukoma ukatakaswa.

4Kisha Yesu akamwambia: Tazama, usimwambie mtu! Ila uende, ujionyeshe kwa mtambikaji, ukitoe kipaji, Mose alichokiagiza, kije kinishuhudie kwao.Mkubwa wa Kapernaumu.(5-13: Luk. 7:1-10.)

5Yesu alipoingia Kapernaumu, mkubwa wa askari akamjia, akambembeleza akisema:

6Bwana, mtoto wangu amelala nyumbani, anaumia vibaya kwa kulemaa.

7Yesu akamwambia: Mimi ninakuja kumponya

8Lakini yule mkubwa wa askari akamjibu akisema: Bwana, hainipasi, uingie kijumbani mwangu, ila sema neno tu! ndipo, mtoto wangu atakapopona!

9Kwani nami ni mtu wa serikali, ninao askari chini yangu. Nami nikimwambia huyu: Nenda! basi, huenda; na mwingine: Njoo! huja; nikimwagiza mtumishi wangu: Vifanye hivi! huvifanya.

10Yesu alipoyasikia akastaajabu, akawaambia waliomfuata: Kweli nawaambiani: Kwa Waisiraeli sijaona bado mtu mwenye kunitegemea kama huyu.Mkwewe Petero.(14-17: Mar. 1:29-34; Luk. 4:38-41.)

14Ikawa, Yesu alipoingia nyumbani mwa Petero, akamwona mama ya mkewe Petero, amelala kwa kuwa na homa.(18-22: Luk. 9:57-60.)

18Lakini Yesu alipoona, watu wengi wakimzunguka, akaagiza, wavuke kwenda ng'ambo.Upepo wa baharini.(23-27: Mar. 4:36-41; Luk. 8:23-25.)

23*Alipoingia chomboni, wanafunzi wake wakafuatana naye.

24Mara kukawa na msukosuko mkubwa baharini, hata chombo kilifunikizwa na mawimbi, lakini yeye alikuwa amelala usingizi.

25Ndipo, walipomjia, wakamwamsha wakisema: Bwana, tuokoe, tunaangamia!

26Yesu akawaambia: Mbona mnaogopa hivyo? Mbona mnanitegemea kidogo tu? Kisha akainuka, akaukaripia upepo na bahari, kukawa kimya kabisa.Mat. 14:31; 16:8; Sh. 107:23-31.

27Lakini watu wakastaajabu wakisema: Ni mtu gani huyu, ya kuwa hata upepo na bahari zinamtii?*

Wenye pepo kwa Wagadara.(28-34: Mar. 5:1-17; Luk. 8:26-37.)

28Alipofika ng'ambo katika nchi ya Wagadara, watu wawili waliopagawa na pepo wakakutana naye wakitoka penye makaburi, ni wakorofi mno; kwa hiyo mtu hakuweza kuipita njia ile.

29Mara wakapiga kelele wakisema: Tuko na jambo gani sisi na wewe, mwana wa Mungu? Umejia hapa kutuumiza, siku zetu zikiwa hazijatimia bado?Luk. 4:41; 2 Petr. 2:4.

30Mbali yao kulikuwako kundi la nguruwe wengi waliokuwako malishoni.

31Wale pepo wakambembeleza wakisema: Ukitufukuza, tutume, tuliingie lile kundi la nguruwe!

32Yesu alipowaambia: Haya! Nendeni! ndipo, pepo walipowatoka, wakawaingia nguruwe. Mara kundi lote likatelemka mbio mwambani, wakaingia baharini, wakafa majini;

33lakini wachungaji wakakimbia, wakaenda zao mjini, wakayatangaza yote, hata mambo ya wenye pepo.

34Mara watu wa mji wakatoka wote, wakutane na Yesu. Walipomwona wakambembeleza, atoke mipakani kwao.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help