1Ahabu akamsimulia Izebeli yote, Elia aliyoyafanya, na jinsi alivyowaua wafumbuaji wote wa Baali.Elisa anamfuata Elia kuwa mwanafunzi wake.
19Alipoondoka huko akamwona Elisa, mwana wa Safati, akilima na ng'ombe, jozi 12 zilikuwa mbele yake, naye alikuwa pale penye ile ya kumi na mbili; Elia akamwendea, akamtupia kanzu yake.
20Ndipo, alipowaacha ng'ombe wake, akamkimbilia Elia, akamwambia: Nipe ruhusa, kwanza ninoneane na baba na mama! Kisha nitakufuata. Akajibu: Nenda, uridi upesi! Usisahau niliyokutendea!Luk. 9:61.
21Aliporudi, amfuate, akachukua ng'ombe wawili, akawaua; kisha akazipika nyama zao na kuvitumia vyombo vya hao ng'ombe kuwa kuni; hizo nyama zao akawagawia watu wake, wazile. Kisha akaondoka, akamfuata Elia na kumtumikia.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.