Mifano 23 - Swahili Roehl Bible 1937

Mafundisho yampasayo mtu amchaye Mungu.

1Ukikaa chakulani kwa mtawalaji

sharti umtambue yeye aliopo usoni pako.

2Jibandikie kisu kooni pako

wewe ukiwa mwenye tamaa ya kula sana!

3Usivitamani vilaji vya urembo vya mwingine!

Kwani ni vyakula vya udanganyifu.

4Usijisumbue kupata mali nyingi,

ukaacha kuutumia utambuzi wako kwa ajili ya hizo mali!

5Au sivyo? Ukizitupia macho yako, basi, haziko tena,

nazo hujitengenezea mabawa kama ya tai ya kurukia kwenda mbinguni.

6Usile chakula chake mwenye jicho baya,

wala usivitamani vyakula vyake vya urembo!

7Kwani yeye ni kama mtu ahesabuye yote rohoni mwake;

hukuambia: Haya! Ule, unywe! lakini moyo wake hauko kwako.

8Kwa hiyo utakitapika kitonge, ulichokila,

nayo maneno yako yapendezayo yatakuwa umeyasema bure tu.

9Usiseme masikioni pa mpumbavu!

Kwani atayabeza maneno yako, uliyoyasema kwa akili.

22Msikie baba yako aliyekuzaa!

Usimbeze mama yako, akiwa mzee!

29Ni nani aliaye? Ni nani apigaye kite?

Ni nani apatwaye na magomvi? Ni nani aombolezaye?

Ni nani ajiumizaye bure? Ni nani aliye na macho mekundu?

30Ndio wao wanaokunywa mvinyo usiku kucha,

ndio wao watembeao kutafuta vileo vikali.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help