Mashangilio 61 - Swahili Roehl Bible 1937

Kumwombea mfalme.Kwa mwimbishaji, auimbishe na kupiga zeze. Wa Dawidi.

1Mungu, lisikie lalamiko langu!

2Yaitikie nikuombayo!

3Kwenye mapeo ya nchi ninakuita, moyo wangu ukizimia. Unikweze mwambani! Kwani ni mrefu wa kunishinda.

4Kwani kimbilio langu ndiwe wewe, u mnara wenye nguvu machoni pao adui.Sh. 18:2-3; 71:3.

5Ninataka kuwamo katika kituo chako kale na kale, na kulikimbilia ficho lililomo mabawani mwako.Sh. 63:3.

6Kwani wewe, Mungu, umeyasikia niliyokuapia, ukanigawia fungu lao waliogopao Jina lako.

7Unamwongezea mfalme siku kwa siku, miaka yake iwe ya vizazi na vizazi.Sh. 21:5.

8Akiendelea machoni pake Mungu atakaa kale na kale. Agiza vya upole na vya kweli, vimsimamie!2 Sam. 7:16.

9Hivyo nitaliimbia Jina lako kale na kale na kuyalipa siku kwa siku niliyokuapia.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help