1Watu wa Efuraimu wakamwuliza: Kwa nini umetufanyizia hivi, usituite, ulipokwenda kupigana na Wamidiani? Wakamgombeza kwa nguvu.Wana wa Gideoni na kufa kwake.
29Kisha Yerubaali, mwana wa Yoasi, akaenda zake kukaa nyumbani kwake.
30Yeye Gideoni akapata wana 70, aliowazaa, kwani alikuwa na wanawake wengi.
31Hata suria aliyekaa Sikemu akamzalia mwana, naye akamwita jina lake Abimeleki (Baba ni Mfalme).
32Gideoni, mwana wa Yoasi, akafa, mwenye uzee mwema, akazikwa kaburini mwa baba yake Yoasi kule Ofura kwa Abiezeri.Waisiraeli wanamwacha Mungu tena.
33Gideoni alipokwisha kufa, wana wa Isiraeli wakamfanyia Mungu ugoni tena na kuyafuata Mabaali, wakamtumia Baali la agano kuwa mungu wao.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.